Breaking News

WAZIRI KAIRUKI: ZAIDI YA NAFASI 10,184 ZIMETANGAZWA KUZIBA PENGO LA WALIOBAINIKA KUWA NA VYETI FEKI.

Serikali imetenga zaidi ya shilingi bii 605 za nyongeza katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18 kwa ajili ya watumishi waliopandishwa na wanaotarajiwa kupandishwa vyeo pamoja na ongezeko la mshahara.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti Utumishi wa Umma na Utawala bora Mhe.Angela Kairuki amesema hayo jijini dare s salaam wakati akifungua semina elekezi kwa watumishi wa umma waliopandishwa  na kukabidhiwa barua za kupandishwa vyeo lakini zoezi hilo likasitishiwa kutokana na zoezi la uhakiki wa vyeti.

Alisema fedha hizo pia zitalipa malimbikizo ya mishahara kwa watumishi hao pamoja na kuwezesha kutekeleza zoezi zima la ajira mpya ambazo zimetangwa tayali na serikali. “Tayari serikali imetoa kibali cha kuajiri watumishi 10,184 kwaajili ya kuziba pengo la watumishi walioondolewa baada ya kugundulika na vyeti feki” alisema Waziri kairuki.
Aidha waziri ametoa agizo kwa wakuu wa taasisi zote za umma kuaajili wale ambao tayali wameshahakikiwa ili kuepuka kuajili watumishi wasiokidhi vigezo vinavyotakiwa kama wenye vyeti feki kufanya hivyo kutaathiri utendaji kazi.


No comments