Breaking News

MHE SAMIA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA MIAKA 100 YA CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA.

Skauti mkuu Bi. Mwantum Bakari Mahiza akifafanua jambo pembeni yake ni eline Kitaty Kamishna Mtendaji wa chama cha skauti Tanzania.

Dar es salaam
Makamu wa Rais Mh.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kuadhimisha miaka 100 ya tangu kuanzishwa skauti Tanzania ambayo yatafanyika kuanzia tarehe 21 hadi 29  Julai mwaka 2017 mkoani Dodoma katika ukumbi wa chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Skauti mkuu Bi. Mwantum Bakari Mahiza alisema ufunguzi wa maadhimisho hayo ambayo yatafunguliwa rasmi tarehe 26 mwezi huu yatawakutanisha skauti zaidi ya elfu nne kutoka mikoa yote  ya Tanzania Bara na Zanzibar.

ALisema pia washriki ktoka katika nchi jirani za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya kidemocrasia ya kongo na kutoka nchi zingne barani afrika, Asia na Ulaya utajadili mambo mbalimbali ikiwemo changamoto wanazokutana nazo katika kipindi cha miaka 100.

Aidha Bi mahiza aliongeza kuwa maadhimisho hayo yatahitimishwa kwa kufungwa siku ya tarehe 28 mwezi huu na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Kassim Majaliwa

Maadhimisho hayo yamepewa Kauli mbiu ya maadhimisho ya skauti ni "Kuwajenga Vijana kuwa Wazalendo na Kufanya Kazi kwa Bidii kwa Maendeleo ya Nchi"

Chama cha Skauti kilianzishwa mwaka 1905 na badae huko Uingereza na muasisi Lord Baden-Powell na baadae kiliingia Zanzibar na hatimae Tanganyika mwaka1917.

No comments