Breaking News

MEYA ISAYA MWITA:WATANZANIA TUJIEPUSHE NA TABIA YA KUBAGUANA KIITIKADI ZA VYAMA, DINI NA KABILA BAADALA YAKE WAENDELEZE UMOJA, UPENDO NA MSHIKAMANO.

Image result for meya mwita
MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema Watanzania wanapaswa kujiepusha na tabia ya kubaguana kiitikadi za vyama, dini na kabila baadala yake waendeleze umoja, upendo na mshikamano.

Mwita, alitoa kauli hiyo jijini hapa jana, wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa jengo la Kanisa la kisasa la Tanzania Assemblies Of God (TAG) lililopo Kivule ,Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jijini.

Alisema kuwa amefikia hatua hiyo baada ya kubain mambo mbalimbali ambayo yameanza kujitokeza nchi ambapo kama Watanzania, watashirikiana na viongozi wa dini katika kusimama na kuliombea Taifa anaamini viashiria vyote vyenye kuashiria vunjifu wa sheria vitatoweka na nchi ikibaki kuendelea na umoja na mshikamano.

"Tangu nimezaliwa sijawahi kushuhudia vita, machafuko katika nchi yetu, kikubwa huwa naona amani iliyotawala, Upendo, na umoja , sasa nawasishi sana ndugu zangu tuendelee kuwa wamoja tusibaguane, kwa namna yoyote ile , ili nchi yetu iendelee kuwa na amani.

"Baba wataifa Hayati Mwalim Julius Nyerere enzi ya uhali wake alikuwa akisisitiza sana kulinda amani ya nchi yetu, na sisi ambao tupo hai hadi sasa , mambo ya vyama, Udini, Ukabila tuweke pembeni tusimame kama Taifa moja,"alisema Mwita.

Awali akijibu risala iliyoandaliwa na uongozi wa kanisa hilo, Mwita aliahidi kuchangia katika ujenzi huo mifuko 100 ya saruji na kiasi cha fedha sh 500,000 huku akiwataka waumini wa kanisa hilo kujitolea ili kufanikisha ujenzi huo.


Katika risala hiyo, ilieleza kuwa sh. Mil. 95 zinahitaji katika kukamilisha ujenzi wa kanisa la kisasa ambalo litakuwa na uwezo wa kuchukua waumini 600.

No comments