Breaking News

CHAMA CHA ADC CHAMWOMBA RAIS KUONDOA KATAZO LA KUTOFANYA MIKUTANO YA KISIASA NA KUTOA NENO KWA CHADEMA KUACHA KUINGILIA MGOGORO WA CUF.

Katibu mkuu wa chama cha ADC-Dira ya Mabadiliko Bw. Doyo Hassan Doyo akiongea katika mkutano na waandishi wa habari, pembeni yake ni Naibu katibu mkuu Bi. Queen Sendiga.


Dar es salaam.
Chama cha alliance for democratic change (ADC), Dira ya Mabadiliko kimemwomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kuondoa katazo kwa vyama vya siasa nchini kutofanya mikutano ya kisiasa na makongamano kwani vyama hivyo vipo kwa mujibu wa sheria za nchi.

Akizungumza jijini Dar es salaam kuelekea kilele cha miaka mitano tangu kuanzishwa katibu mkuu wa chama cha Hicho Bw, Doyo Hassan Doyo alisema katazo hilo la kutofanya mikutano ya kisiasa nchini limekuwa na athari sana kwa vyama vichanga ambavyo havina wabunge, madiwani na  wenyeviti wa serikali za mitaa.

Alisema chama cha ADC kimwomba mhe Rais Magufuli kuondoa katazo hilo kwani ni haki ya chama cha siasa kwa mujibu wa sheria kuendesha shughuli zake kwa njia ya mikutano ambapo wamekuwa wanadi sera za vyama vyao kwa wananchi.

“katazo la kuzuia kufanya mikutano kwa vyama vya siasa na kutoa nafasi kwa wabunge na madiwani ambao wamechaguliwa kuendesha mikutano katika maeneo yao ni kuvidhoofisha vyama vichanga ambavyo havina wabunge, madiwani na viongozi wa serikali za mitaa” Alisema Bw. Doyo.

Akiongelea mgogoro unaoendelea ndani ya chama cha wananchi CUF kati ya mwenyekiti anayetambuliwa na msajili Prof Lipumba na katibu mkuu wake Maalim Seif ameshauri viongozi hao kukaa pamoja na kumaliza tofauti zao.

Alisema kushindwa kupatia ufumbuzi wa haraka mgogoro huo jambo hilo litapelekea wanachama wao kukata tamaa hivyo kutishia Uhai wa chama hicho pamoja na kuviathili vyama vingine vya upinzani nchini.

Aidha Bw. Doyo ametoa onyo kwa chama cha democrasia na maendeleo (CHADEMA) kuacha mara moja kuingilia mgogoro unaoendelea ndani ya CUF kwani kwa kufanya hivyo kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani pia ni kukiuka sheria na taratibu za vyama vya sasa.

Pia chama cha ADC kimempongeza Rais magufuli kwa hatua ambazo amekuwa akizichukua kuhakikisha analinda asilimali za nchi hususani madini pamoja na bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kupitisha sheria mpya ya madini ambayo itasaidia kupunguza ubathilifu wa asilimali hiyo ya taifa.

Katika hatua nyIngine chama cha hicho kimelaani mauaji ya raia yanayoendelea kuripotiwa mkoani Pwani na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano wa hali na mali kwa vyombo vya ulinzi na usalama hili wahusika wapatikane na kuchukuliwa hatua za kisheria kwani jambo hilo ni la kitaifa sio chama kimoja cha siasa.

Chama cha ADC dira ya mabadiliko kinatajia kuadhimisha miaka mitano tangu kuanzishwa kwake ambapo chama kitaadhimisha kwa kufungua matawi, kutembelea wanachama wake pamoja na taasisi mbalimbali.

No comments