TRA YAFUNGA MADUKA YA WAFANYABIASHARA WASIOTUMIA MASHINE ZA EFD KARIAKOO
Afisa wa Kampuni ya Yono Auction Mart
(kulia) na mmoja wa wafanya biashara wakifunga makofuli kwenye duka la madera
katika mtaa wa Congo Kariakoo Dar es Salaam.
Wafanya biashara waliokamatwa eneo la
Kariakoo Mtaa wa Congo Dar es Salaam, wakifunga maduka kufatia kukutwa na kosa
la kutoitikia wito wa mamlaka hiyo kwenda kulipia faini kutokana na utoaji wa
huduma pasipo kutoa risiti za kielektoniki licha ya kuwa na mashine wakifunga
duka lao walipokamatwa na maofisa wa TRA.
Afisa wa Mamlaka ya Mapato Nchini
(kushoto) akisubiri mmiliki wa duka la urembo lililokutwa likiendelea kufanya
biashara hata baada ya kukutwa wakiuza bidhaa zao pasipo kutoa risiti za
kielekroniki licha kuwa na machine inayotakiwa kutumika kwa utoaji wa risiti
kwa wateja wao iliyotolewa na TRA.
Afisa wa Kampuni ya Yono Auction Mart akikagua
moja ya duka la wafanyabiashara katika Mtaa wa Aggrey Kariakoo Dar es Salaam
wakifanya biashara bila pasipo kutoa risiti ya kielektoniki licha ya kuwa na
mashine hiyo.
Afisa wa Kampuni ya Yono Auction Mart
akifunga kofuli kwenye lango duka la wafanya biashara waliokamatwa katika Mtaa
wa Aggrey Kariakoo Dar es Salaam wakifanya biashara bila pasipo kutoa risiti ya
kielektoniki licha ya kuwa na mashine.
Dar es salaam:
Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) imeendelea
kufanya zoezi la ukaguzi wa maduka ya wafanya biashara wanaouza bidhaa zao
pasipo kuwapatia risiti za mashine za Kielektroniki (Efd) jijini Dar es Salaam.
Kampeni hiyo imeendelea kufanyika katika
eneo la Kibiashara la Kariakoo na itakuwa endelevu kuhakikisha wafanya biashara
wanazingatia sheria, kanuni na taratibu za biashara katika mauzo ya bidhaa zao.
Afisa wa Kampuni ya Yono Auction Mart ambao wanaendesha zoezi hilo kwa kushirikiana na
jeshi la Polisi wakisimamia duka la mfanyabiashara waliokutwa wakiendelea kutoa
huduma ilhali awali walikutwa wakiuza bidhaa hizo pasipo kutoa risiti ya
kielektoniki licha ya kuwa na mashine.
Hatua ya ukamatwaji kwa wafanya biashara
hao inatokana na kitendo cha kutokuitikia wito wa mamlaka ya Mapato Nchini
(TRA) wa kwenda kulipa faini baada kufanya kosa hilo.
Kwa kosa hilo watalazimika kulipa kati ya
shilingi milioni 3 mpaka 4 na nusu ili waruhusiwe kuendelea na biashara.
(Picha zote na Robert Okanda Blogspot)
No comments