DC MGANDILWA AFUNGA VIWANDA VYA WACHINA KIGAMBONI, KUFUATIA UKWEPAJI WA KODI ZA SERIKALI
Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Mhe Hashim Mgandilwa, leo tarehe
20/6/2017 amefanya ziara ya kushtukiza katika kiwanda cha plastic cha Ruider
Plastic Limited kinachomilikiwa na raia mwenye asili ya China.
DC
Mgandilwa aliyeambatana na Mkurugenzi wa manispaa ya Kigamboni Ndg Steven
Katemba, walikagua na kugundua mambo mbalimbali yakiwemo ya kiwanda hicho
kuendesha shughuli zake pasipo kufuata taratibu za nchi kikamilifu na baadhi ya
mianya ya ukwepaji wa kodi.
Baada ya kutembelea eneo la kiwanda ili kujionea shughuli za
uzalishaji, Msafara huo ulioongozwa na DC Mgandilwa ulibaini kuwa katika eneo
hilo kuna viwanda tofauti Saba vinavyozalisha bidhaa tofauti tofauti.
Viwanda vilivyobainika ni pamoja na kiwanda cha kutengeneza mabomba
ya maji ya plastic, kiwanda cha kutengeneza mikeka, kiwanda cha kutengeneza
bodi za dari (Ceiling board), kiwanda cha kutengeneza mifuko ya plastic,
kiwanda cha kutengeneza maboksi ya plastic kwa ajili ya kutunza vitu vya
baridi, kiwanda cha kuyeyusha chupa za plastic, na kiwanda cha kutengeneza mito
ya kulalia.
Viwanda vyote hivyo Saba vinafanya shughuli za uzalishaji katika
eneo moja na huku kiwanda kinacholipa kodi za serikali kikiwa ni kimoja tu
nacho kikisuasua kulipa kama inavyostahili.
Baada ya kutembelea viwanda vyote hivyo, DC Mgandilwa amewataka
wamiliki wa viwanda hivyo kusitisha uzalishaji wake mara moja leo hii.
DC Mgandilwa amesema kusimama kwa shughuli za uzalishaji unatoa
mwanya kwa timu kutoka mamlaka ya mapato (TRA) na Manispaa ya Kigamboni ambao
amewaagiza kuweka kambi katika viwanda hivyo kuanzia kesho ili kupitia nyaraka
zote na kubaini kiasi cha mapato ambayo serikali imekuwa ikiyapoteza tangu
waanze uzalishaji.
DC Mgandilwa ameagiza kuwa baada ya tathimini hiyo kukamilika
pesa yote ambayo serikali imekuwa ikipoteza tangu kuanzishwa kwa viwanda hivyo
ilipwe mara moja iwezekanavyo na ndipo uzalishaji uendelee kwa kufuata taratibu
zote za serikali.
Inakadiriwa kuwa kiwanda kimoja kilitakiwa kulipa Sh 101 milion
kwa mwezi hivyo kuifanya serikali kupoteza mapato ya zaidi ya Shilingi Milioni
700 kwa mwaka.
No comments