TGNP YAWANOA WANAFUNZI WASICHANA WALIOHITIMU NA KUFAULU VIZURI VYUONI
Mtandao wa Wanawake
Tanzania (TGNP) Changamoto kubwa za
kielimu zinazowakabili wasichana katika safari ya ufaulu wa masomo ni kubwa
ikilinganishwa na wavulana kwakuwa wasichana hubebeshwa majukumu mengi zaidi
ambayo hupunguza muda wao wa kujisomea
Akizungumza wakati wa
hafla ya kuwapongeza wasichana 38 waliofanya vizuri katika elimu ya juu, jijini
Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa (TGNP), Bi Lilian Liundi, alisema wasichana wengi
wanashindwa kufikia malengo kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo
kujiingiza katika masuala ya mapenzi wakiwa bado shuleni na kuwa na mtazamo wa
kwamba wao ni wanyonge.
Alisema wasichana
hawa ambao wamefanya vizuri kutoka katika vyuo mbalimbali pamoja na kuwepo na
changamoto mbalimbali zilizokuwa zinawakabili wameonesha ukombozi kwa wasichana
wenzao kwa kuonyesha kuwa wanaweza kuleta maendeleo ya mwanamke mwezio.
Bi Liundi amefafanua kuwa TGNP imekuwa mstari wa mbele katika kuendesha harakati za kumkomboa mwanamke katika changamoto mbalimbali sambamba na kuendesha semina na warsha mbalimbali ambazo zimekuwa zikijikita zaidi katika jitihada za kumkomboa mwanamke sambamba kuwajengea uwezo.
Bi Liundi amefafanua kuwa TGNP imekuwa mstari wa mbele katika kuendesha harakati za kumkomboa mwanamke katika changamoto mbalimbali sambamba na kuendesha semina na warsha mbalimbali ambazo zimekuwa zikijikita zaidi katika jitihada za kumkomboa mwanamke sambamba kuwajengea uwezo.
Aidha aliongeza kuwa kuendelea
kuwepo na fikra potofu kwa wanawake wengi wamekuwa wakijiona kama wao ni daraja
la pili hali ambayo inafanya kukosa haki zao za msingi na kuendelea kuweka
mfumo dume wa maamuzi kufanywa na wanaume.
Kwa upande wake Mmoja
wa wahitimu wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji, bi Aisha Soudy alisema wasichana
wanakabiliana na changamoto nyingi moja wapo ni kuendelea kuwepo kwa mila na
tamaduni ambazo humpendelea mtoto wa kiume huku mtoto wa kike akionekana
asiyeweza kufanya kitu,
Naye mhitimu aliyefanya vizuri katika matokeo ya Chuo Kikuu cha Dodoma, Sara Mgonela alisema msichana ana nafasi yake kama akijitambua anachokifanya katika jamii yake.
Naye mhitimu aliyefanya vizuri katika matokeo ya Chuo Kikuu cha Dodoma, Sara Mgonela alisema msichana ana nafasi yake kama akijitambua anachokifanya katika jamii yake.
Alisema
licha ya kuwepo changamoto nyingi kama mtoto wa kike aliweza kufanya vizuri na
kuwataka wasichana kujiamini kuwa wanaweza na kuwa na bidii.