Breaking News

UNFPA YATOA ELIMU KWA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU FISTULA

Waandishi wa habari wametakiwa kujikita zaidi kuandika habari ambazo zitasaidia kuijengea uelewa jamii juu chanzo na dalili za ugonjwa wa fistula ambao chanzo chake kikubwa ni Uzazi usio salama.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semeni ya siku moja ya kutokomeza fistula duniani kwa waandishi wa habari jijini Dar es salaam mwakilishi wa shirika la umoja wa kimataifa la idadi ya ya watu duniani (UNFPA) nchini na Dkt Hashina Begum alisema bado juhudi za pamoja zinahitajika hasa elimu kwa jamii juu ya ugonjwa huo.
Alisema shirika hilo kwa kushirikiana na serikali na wadau mbalimbali wa sekta ya afya wamekuwa wakitoa elimu kwa juu ya chanzo cha ugonjwa fistula, madhara yake pamoja na matibabu ya ugonjwa huo  sambamba na njia sahihi za kujinga na ugonjwa huo.

Dkt Begum aliongeza katika kuakikisha wanatokemeza ugonjwa huo duniani UNFPA tayali imeshatoa mafunzo kwa wakunga elfu nne ambayo kwa lengo la kutokomeza ugonjwa huo sambamba na kuzuia vifo vya wanawake na watoto wakati wa uzazi pamoja na kuwashauri wajawazito kuwa na utamaduni wa kuwahi vituo vya afya mapema ili kupunguza tatizo hilo.
“katika kuhakikisha fistula inatokomezwa duniani ni vema matunzo ya lishe bora yaanzie utotoni ili kusaidia ukuaji bora wa nyonga ambayo itasaidia kuepukana na fistula ukubwani” alisema Dkt Begum

Kwa upande wake mtoa mada kutoka chama cha wakunga Tanzania (TAMA), Bi Martha Rimoyi alisema kwa mujibu wa takwimu zinaonyesha kuwa vifo vya wanawake wajawazito vimeongezeka kutoka 454 hadi kufikia 556 kwa kila vizazi hai laki moja kila mwaka.

Kwa takwimu hizo inaonekana inatakiwa juhudi za pamoja hususani katika kutoa elimu juu ya ugonjwa wa fistula kwa hili kusaidia jamii kutambua njia sahihi ya kujikinga na ugonjwa huo ambao umekuwa ikiondoa utu na kusema ni wakati wa kuirejesha heshima kwa wanawake.
Alisema duniani kote kunakadiliwa kuwa na wanawake na wasichana wagonjwa wa fistula milioni mbili na kila mwaka kuna wastani wa wagonjwa wapya kati ya 50,000 hadi 100,000 na wanaopata matibabu ni 20,000 pekee.

Kilele cha siku ya Tokomeza Ugonjwa wa fistula duniani uazimishwa kila mwaka 23 mwezi mei ambapo mwaka huu shirika la idadi ya watu duniani (UNFPA) limeandaa mafunzo ya kutokomeza fistula duniani kwa kushirikiana na wadau wa afya CCBRT na AMREF.
 c