IITA YAWANOA WANAFUNZI WAPENDE MASOMO YA SAYANSI
Mkurungenzi
wa Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa kilimo cha kitropiki Tanzania (IITA) Dkt Victor
Manyong akiongelea maadhimisho ya siku ya kilimo duniani ambapo nchini
imeadhimishwa kwa kuwakutanisha wanafunzi kutoka shule mbalimbali kuwajengea
hali ya kupenda masomo ya sayansi mapema leo jijini Dar es salaam.
Mkuu wa kitendo cha
mawasiliano wa Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa kilimo cha kitropiki Tanzania
(IITA),Bi, Catherine Njuguna akitoa ufafanuzi kuhusu maadhimisho ya siku ya
kilimo duniani mapema leo jijini Dar es salaam
Mmoja
ya watafiti wa Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa kilimo cha kitropiki Tanzania
(IITA) akitoa maelekezo jinsi taasisi hiyo inavyoendesha shughuli zake za
kiutafiti kwa wanafunzi kutoka shule mbalimbali mapema leo Jijini Dare s salaam.
Dar es Salaam
Taasisi
ya kimataifa ya utafiti wa kilimo cha kitropiki (IITA) leo imeadhimisha siku ya
umuhimu wa mimea duniani kwa kusherehekea na watoto wa shule ili waweze
kujifunza masomo ya kisayansi kwa bidii.
Akizungumza
katika maadhimisho hayo mkurugenzi mtendaji taasisi ya kimataifa ya utafiti wa ya
kilimo cha kitropika (IITA), Bw.Victor
Manyong alisema taasisi hiyo imekuwa ikijishughulisha na utafiti wa kilimo ili kuwasaidia wakulima
katika mchakato wa kilimo na ndiyo mana siku hii hushirikisha watoto ambao ni
vema wakipata mafunzo tangu awali ili kufikia mafanikio ya kisayansi.
Mkurugenzi
Manyong amesema kuwa changamoto mbalimbali zimekuwa zikiwakabili wakulima kwa
kukosa vitendea kazi vya kisasa pamoja na upungufu wa pembejeo na mbegu.
kwa
upande wake afisa mawasiliano wa Taasisi hiyo Bi Catherine Njuguna alisema matokeo
ya tafiti zao ambazo wamekuwa wakifanya sehemu mbalimbali nchini wamegundua
kuwepo na changamoto nyingi sana hususani magonjwa ya mimea.
alisema
pamoja na wataalamu kushauri juu ya njia bora za kutumia kwa wakulima hususani
wadogo bado kumekuwepo na mwamko mdogo kwao hususani katika swala la matumizi
sahihi ya pembejeo pamoja na ushauri wa wataalam wa kilimo.
Maadhimisho
ya siku ya umuhimu wa mimea duniani huadhimishwa tarehe 14 mwezi mei.
No comments