Breaking News

DC MJEMA AMWAGIA SIFA RAIS MAGUFULI

Mkuu wa wilaya ya Ilala Mhe.Sophia Mjema ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  kwa kutoa fursa adhimu ya kukimbiza  mwenge wa Uhuru katika wilaya yake sambamba  na kuzindua  pamoja na kuhamasisha shughuli mbalimbali za maendeleo.

Mh.Mjema  amesema kuwa kwa kuzingatia hoja na vipaumbele vya serikali ya awamu ya tano Mwenge wa Uhuru  wa mwaka 2017 umebeba kauli mbiu  isemayo “Shiriki kukuza Uchumi wa Viwanda kwa Maendeleo ya nchi yetu” ambapo katika kutimiza azma hiyo ya serikali ya manispaa ya Ilala imewewka mikakati shirikishi ya uanzishaji, uendelezaji na usimamizi wa viwanda ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya maendeleo ya 2025.

Mh. Mjema amesema kuwa halmashauri ya manispaa ya Ilala imetenga zaidi yay a hekta 289 ili kuanzisha maeneo maalum kwaajili ya uwekezaji (EPZ)  na kuyataja maeneo hayo kuwa ni Bonde la Msimbazi,Tabata,Luhanga,Kiboga na Msongola, Bangulo, Mji mpya Majohe, Yongwe, Chanika na Vingunguti sambamba na kutenga mitaa ya viwanda vidogovidogo kama vile Gerezani

Aidha Mjema amesema kuwa kwa pamoja wanaunga mkono vita dhidi ya dawa za kulevya  pamoja na kuhakikisha vitendo vya rushwa vinatokomezwa nchini.


Mkuu wa Ilala Mh.Mjema amebainisha mwenge wa Uhuru unapitia jumla ya miradi tisa ya maendeleo ambapo shughuli za kuweka mawe ya msingi, kukagua na kuzindua miradi hiyo yote ina jumla ya thamani ya shilingi zaidi ya Bilioni 14.