Breaking News

HUU NDIO MTIZAMO WA JUKWAA LA KATIBA TANZANIA JUU YA BAJETI YA SERIKALI KWA MWAKA 2016/17, PAMOJA NA KWAMO WA MCHAKATO WA KATIBA MPYA

Mkurugenzi mtendaji  wa jukwaa la katiba Bw. Hebron Mwakagenda akifafanua jambo mapema leo jijini dar es salaam

Na Frank wandiba
Jukwaa la katiba Tanzania (JUKATA) limebaini utekelezaji duni wa bajeti ya mwaka 2016/2017 hasa katika miradi ya kimaendeleo ambapo wamebaini kuwa serikali imepanga kutumia shilingi trilioni 29.5 katika mwaka wa fedha 2016/17.

Akizungumza  na waandishi  wa habari mapema leo jijini dar es salaam mkurugenzi mtendaji  wa Jukwaa la katiba Bw. Hebron Mwakagenda amesema katika bajeti ya serikali kwa miradi ya maendeleo kwa mwaka unaoelekea mwishoni ilikuwa trillion 11.8 sawa na asilimia 40 ya bajeti kuu ambapo hadi kufikia mwezi machi 2017 miezi mitatu kabla ya utekelezaji  wa bajeti kukamilika serikali imepeleka shilingi trilioni 3.5  tu ambayo ni sawa na asilimia 34 ya fedha zilizopangwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo 2016/17.

Mwakagenda amesema  kufuatia mwenendo huo hafifu wa utekelezaji wa bajeti  umetoa taswira ya wazi kuwa serikali inaweza isitekeleze bajeti ya maendeleo kwa kiwango cha asilimia 50 hadi kufikia mwisho wa mwaka wa bajeti ambao ni mwezi julai hivyo kupeleka bajeti ya mwaka 2017/18 yenye mwendelezo kama huo kutotekelezeka hivyo kufanya azma ya Tanzania ya viwanda kushindwa kufikiwa.

Bw. Mwakagenda ametoa pongezi kwa Prof Palamagamba Aidan Kabudi  kwa kuteuliwa kuwa waziri wa katiba na sheria kwani anao ujuzi wa kutosha pasi shaka yeyote kuongoza wizara hiyo muhimu na nyeti pamoja na ushiriki wake akiwa kamishna wa tume ya mabadiliko ya katiba mpya hivyo amepitia uzoefu ambao utasaidia katika kuelekea mchakato wa katiba mpya ambao haupo bayana.

Aidha JUKATA limepokea mtizamo chanya kuhusu taarifa kwamba serikali ya awamu ya tano ina mpango wa kuendelea na mchakato wa kuandika katiba mpya kwa mujibu wa kauli ya waziri wa sheria na katiba Prof Kabudi aliyoitoa kwa wabunge wa kamati ya bunge ya na katiba na sheria kwamba serikali inatarajia kuanza marekebisho ya sheria ili kukamilisha mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya.

Ameongeza kuwa mchakato wa kuipata katiba mpya ulisimama na na zipo changamoto kuu mbili ambazo ni busara kuzitafutia ufumbuzi kabla ya kuendelea ili kuweza kupata katiba mpya ambayo ni sheria  ya mabadiliko  ya katiba namba nane ya mwaka 2011 (pamoja na marekebisho yake) na sheria ya kura ya maoni ya mwaka 2013.


No comments