Breaking News

MTANDAO WA MASHIRIKA YANAYOPINGA NDOA ZA UTOTONI WATOA TAMKO KUFATIA KUWEPO KWA TAARIFA SERIKALI KUKATA RUFAA JUU YA KESI KUPINGA NDOA ZA UTOTONI



Mwenyekiti wa mtandao wa kuzuia ndoa za utotoni Bi Valeria Msoka akisoma tamko hilo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani)akisoma tamko la mtandao huu.

Mwenyekiti wa mtandao wa kuzuia ndoa za utotoni Bi Valeria Msoka akisoma tamko hilo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani)Kushoto kwake Mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za binadambi hellen kijo Bisimba na Bi, Rebeca Gyumi mkurugenzi mtendajiwa tasisi ya wasichana Initiative

Na Frank Wandiba
 
Mtandao wa mashirika yanayopinga ndoa za utotoni   nchini umeitaka ofisi  ya mwanasheria mkuu wa serikali kuondoa kusudio la kukata rufaa juu ya kesi ya kupinga ndoa  za utotoni  iliyotolewa hukumu  kuitaka serikali kuondoa baadhi ya vifungu vya sheria ya ndoa  ambavyo vinaruhusu mtoto wa kike kuolewa akiwa na umri chini ya miaka 18.

Akisoma tamko hilo mbele ya waandishi wa habari mwenyekiti wa mtandao huo Bi Valeria Msoka  amesema mtandao huo ushitushwa , kushangazwa na kusikitishwa  na taarifa iliyotolewa na mwanasheria mkuu wa serikali kuwa serikali natarajia kukata rufaa kufatia hukumu iliyotolewa na mahakama kuu ambayo iliyokuwa inahoji uhalali wa kikatiba wa kifungu namba 13 na 17 vya sheria ya ndoa ya mwaka 1971.

Amesema kufatia hukumu hiyo ambayo ilielekeza  serikali  kuanza mchakato wa kubadili vifungu hivyo ndani ya mwaka mmoja  kuanzia kutolewa kwa hukumu hiyo zipo taarifa kuwa mwanasheria mkuu wa serikali anafikilia kukata rufaa kupinga hukumu hiyo mahakamani.

 Kufatia uhamuzi huo mtandao unashindwa kuelewa rufaa hiyo inabebwa kwa misingi gani au serikali ina mpango wa kuendelea kuwa na vifungu vyahivyo vya kisheria viavyoruhusu watoto wa kike kuolewa chini ya miaka 18 wakati tayali pia waziri mwenye dhamana ya sheria alishatoa kauli bungeni kuwa serikali ipo mbioni kupeleka mswada wa sheria kupinga ndoa za utotoni.

Aidha ameongeza kuwa kitendo cha Mwanasheria mkuu  kukata rufaa kuna ashiria kuwa serikali INA unaunga mkono ndoa za utotoni jambo ambalo lipo kinyumena mkataba wa kikanda na kimataifa wa kulinda haki na ustawi wa mtoto wa kike ulio sainiwa  mwaka 1989 kwa upande wake Koshuma mtegeti ambaye ni mwakilishi wa kulinda utu wa mtoto  ameitaja mikoa ya Tabora na Mwanza nimoja ya mikoa inayo ongoza kwa ndoa za utotoni.

Mapema mwezi uliopita mahakama mkuu ya Tanzania ilitoa hukumu  dhidi ya kesi ya kupinga  vifungu vya sheria  vinavyo ruhusu  mtoto wa kike kuolewa akiwa na umri  chini ya miaka kumi na nane ilyo funguliwa na mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya Msichana Initiative  dhidi ya mwanasheria mkuu wa Serikali.




No comments