Breaking News

WAZIRI UMMY : UJENZI WA MADARASA WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 95

Na: Angela Msimbira-TAMISEMI 
Waziri Wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu amesema ujenzi wa madarasa 15,000  umekamilika kwa asilimia 95 katika mikoa yote  ya Tanzania bara na  maeneo machache hawajakamilisha kutokana na changamoto  mbalimbali ikiwemo  upatikanaji wa malighafi ya ujenzi, uchaguzi wa maeneo ya ujenzi  na hali ya hewa.

Waziri Ummy  amemuhakikisha Rais wa Jamhuro ya Muungano wa Tanzania  kuwa hadi kufikia tarehe 15 januari, 2022 madarasa yatakuwa yamekamilika na wanafunzi wataanza masomo yao.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa  na mapambano  dhidi ya UVIKO -19 Ikulu Jini Dar es salaama Waziri Ummy  amesema  kiasi cha shilingi bilioni 240  ziliidhinishwa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa  12, 000 ya shule za sekondari na bilioni 60 kwa ajili ya ujenzi  madarasa ya shule shikizi za msingi  na shilingi bilioni 4 kwa ajili  ujenzi wa mabweni 50  kwa  wanafunzi wenye mahitaji maalumz

Ameendelea kufafanua kuwa kiasi cha shilingi  bilioni  203.1 zilitolewa kwa ajili ya Sekta ya Afya na bilioni 5  kwa ajili ya kuboresha mazingira  ya kufanyia biashara  kwa wafanyabiashara wadogo.

Amesema  hadi kufikia  tarehe 31 Disemba, 2021 kwa upande wa sekta ya elimu  msingi Ofisi ya Rais TAMISEMI  imepokea shilingi  bilioni 304  ambazo zilikuwa zimetengwa  kwa ajili ya ujenzi  wa madarasa  ya shule za Sekondari  na shule shikizi  jumla 15,000 pamoja na mabweni.

Ameendelea kufafanua kuwa  ujenzi wa madarasa ya shule za sekondari yatawezesha  wanafunzi wote 907,803 waliofaulu mitihani  ya kumaliza darasa la saba  na kuingia kidato cha kwanza  kuanza shule siku moja badala  ya kuwa na awamu tatu  kama ilivyokuwa mika iliyopita

Waziri Ummy amesema kuwa Ofisi ya Rais TAMISEMI  iliomba madarasa 12,000  ikiwa  na makadirio kuwa watoto watafaulu kwa asilimia 90 lakini  matokeo ya mitihani  ufaulu ni asilimi 82  hivyo kuna madarasa ya ziada  2,292  ambayo yatasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi wa vidato vingine katika shule za Sekondari.

Kuhusu ujenzi wa  madarasa  3000 ya shule shikizi Waziri Ummy amesema serikali imewasaidia watoto  wa umri mdogo kutembea umbali mrefu, kupata elimu  katika madarasa mazuri na ya kisasa badala ya madarasa  ya nyasi, yaliyotengenezwa na miti na ambayo hayavutii.

“Kwa upande kwa elimu  msingi tumepokea fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni 50  katika shule  za msingi zenye wanafunzi  wenye mahitaji maalum  ambayo yatasadia kuboresha  mazingira ya watoto wenye ulemavu kuweza kujifunza na kusoma katika mazingira mazuri” amesisitiza Waziri Ummy

Ofisi ya Rais TAMISEMI  imeidhinishiwa  kiasi cha shilingi bilioni 512 kupitia mpango wa maendeleo wa taifa na mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO kwa ajili ya Sekta ya Elimu, Afya na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

No comments