Breaking News

MISA TANZANIA Waichamhua Ripoti ya Sheria Ya Takwimu na Sheria ya Huduma ya Mtandao

Wadau kutoka taasisi za kihabari wamepitia na  kutoa maoni kwenye ripoti ya Sheria ya Takwimu na Sheria ya huduma za mitandao na posta (Statistics Act, 2010 & EPOCA 2018), kwenye kikao kilichofanyika jijini Dar es Salaaam hivi karibuni.

Kikao hicho kilichoandaliwa na MISA TANZANIA kwa ushrikiano wa IMS (INTERNATIONAL MEDIA SUPPORT) Wadau hao walijadili mambo kadhaa yaliyoainishwa kwenye ripoti ikiwemo maeneo mbalimbali ya sheria hizo mbili ambayo yamekuwa kikwazo na changamato kwa tasnia ya habari.
Baadhi ya maeneo yaliyoguswa  na kutolewa maoni na wadau  kutoka katika sheria hizo tajwa na kanuni zake ni pamoja na upitiwaji sheria ndogo/kanuni zinazotungwa na TCRA kwani ndizo zinye vipingamizi na ukinzani mkubwa dhidi ya haki ya kutoa na kupokea taarifa. 

Pia  wadau hao walipendekeza  kwamba ripoti hiyo ijumuishe mabadiliko ya  mfumo unaozita Redio za kijamii na kuzifanya ziwe kwenye mfumo wa kibiashara litakavyoathiri upatikanaji wa taarifa hasa kwa jamii zilizosahaulika.

Maoni yaliyotolewa na wadau wa habari katika kikao hicho yatatumika kuiboresha ripoti tayari kwa kuombea na kupendekeza mabadiliko ya vipengengele ainishwa, hasa kwa wakati huu ambao wizara husika imeonyesha utayari wa kupokea maoni na mapendekezo ya wadau ili kuiboresha tasnia ya habari nchini.
Akizungumza  katika kikao hicho Kaimu Mkurugenzi wa MISA TAN  Andrew Marawiti alisema ripoti hiyo imeandaliwa ili kufanyia udukuzi na uzengezi wa mabadiliko ya baadhi ya maeneo ya sheria hizo yanayoonekana kududumiza uhuru wa upatikanaji na utoaji wa habari nchini

No comments