Breaking News

Vijana Changamkieni Mafunzo Yanazotolewa Na Chuo Cha Taifa Cha Utalii Nchini.

Mkurugenzi mkuu wa bodi ya utalii Tanzania Bi. DEVOTHA MDACHI akiongea wakati wa ufunguzi  wa tamasha la maonyesho ya la taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.

Dar es salaam:
Vijana nchini watakiwa kuchangamkia fursa za mafunzo yanayotolewa na chuo cha taifa cha utalii (NCT) ili kuwawezesha kuweza kutapa ujuzi ambao utawasaidia kuwapatia ajira sambamba na kujiajili wa wenyewe.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa tamasha la maonyesho ya la taaluma katika chuo cha taifa cha utalii jijini Dar Es Salaam kwa niaba ya katibu mkuu wa wizara ya maliasiri na utalii , Mkurugenzi mkuu wa bodi ya utalii Tanzania Bi. DEVOTHA MDACHI alisema vijana wajitokeze kwa wingi kuchangamkia fursa hiyo zinazopatika mara baada ya kuhitimu mafunzo ya yjuzi yanayotolewa na chuo hicho.

“Vijana jitokezeni kuchangamkia fursa zinazotolewa na chuo cha taifa cha utalii kwani zitawasaidia vijana katika kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana, sambamba na kuwaongeza kipato hivyo kuinua uchumi wa nchi kupitia vijana” alisema Bi Mdachi.

Alisema serkali kupitia wizara ya maliasiri na utalii imetoa gari moja dogo ambalo litawasaidia vijana katika kufanikisha utalii wa ndani kuunga mkono jitihada za chuo hicho katika kuendelea kutoa mafunzo yanayokidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.
Mwenyekiti Wa Bodi Ya Ushauri Ya Chuo Cha Taifa Cha Utalii Bi. BENADETA NDUGURU akizungumza wakati wa ufunguzi  wa tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.

Kwa upande wa Mwenyekiti Wa Bodi Ya Ushauri Ya Chuo Cha Taifa Cha Utalii BI. BENADETA NDUGURU alisema wameandaa tamasha hilo kufatia kutambua umuhimu wa vijana katika kujenga uchumi wa nchi sambamba na kuwakutanisha wadau kutoka taasisi mbali mbali zinazojishughulisha na utoaji wa huduma za kupokea watalii, mahoteli, waongoza watalii hili kuweza kujionea namna chuo hicho kinavyo toa mafunzo yake.

Aidha Bi. Ndunguru aliongeza kuwa kupitia tamasha hilo wadau wataweza kujionea jinsi chuo hicho kinavyoendesha shughuli zake hivyo kuwa moja ya njia ya kuwawezesha wahitimu wao chuo hicho kupata ajira kwa urahisi.

Atamasha hilo ambalo limebeba ujumbe usemao "FURSA ZA AJIRA KWA VIJANA KUPITIA TAALUMA YA UKARIMU NA UTALII" ikiwa kama njia ya kuufahamisha uuma juu ya mafunzo yatolewayo katika chuo cha taifa cha utalii.
Mkurugenzi wa chuo cha taifa cha utalii Bi. Sporah  Liana akifafanua jambo katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.



Wadau kutoka taasisi mbali mbali wakiwasilisha mada katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.

Washiriki tamasha hilo kutoka taasisi mbalimbali wakifatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.

Mgeni rasmi katika tamasha la maonyesho ya la taaluma Bi. DEVOTHA MDACHI akisikiliza maelezo kutoka kwa wanafunzi wakati alipotembelea mabanda ya wanafunzi hao kujionea namna shughuli zinazofanywa na kuratibiwa na chuo hicho katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.


Washiriki wa tamasha hilo wakifatilia kwa makini mada ambazo zikiwasilishwa katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.
Mgeni rasmi katika tamasha la maonyesho ya la taaluma Bi. DEVOTHA MDACHI akiwa katika picha ya pamoja na vingozi wa chuo icho pamoja na wadau mbalimbali walioshiriki katika tamasha la maonyesho ya taaluma katika chuo cha taifa cha utalii  (NCT), April 27 2018 jijini Dar Es Salaam.

No comments