Breaking News

Amref Yazindua Mradi Wa Hamasa Katika Uzazi Wa Mpango Mikoa 24 Nchini.

Hali ya uzazi wa mpango nchini bado ni changamoto kubwa kutokana na asilimia kubwa ya wananchi hususani waishio vijijini kuendelea kuzaaa idadi kubwa ya watoto huku kipato chao ni kidogo hali ambayo inawafanya washindwe kuwahudumia.

Akizungumza mapema leo Jijini Dar es salaa, Mkurugenzi wa Amref helth Africa Dkt. Frolence Temu mara baada ya hafla ya uzinduzi wa mradi mpya wa health Systems Advocacy ambao una lengo la kuhamasisha jamaii kutambua namna ya kupanga uzazi pamoja na faida zake.

Dkt.Temu alisema mradi huo ambao unadhaminiwa na serikali ya Uholanzi kwa euro milioni 150 na  unatekelezwa kwa muda wa miaka mitatu katika mkoa wa SHINYANGA kutokana na mkoa huo kuwa na changamoto kubwa ya wananchi kuzaa watoto wengi nakushindwa kuwa patia Huduma za msingi kama vile chakula, malazi.
Mapema akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Msaidizi kitengo cha Afya ya Uzazi wa Mtoto Bw. Machumu Miyeye ambaye ni Mfamasia kitengo cha Afya ya uzazi na mtoto alisema serikali inaendelea kuchukua hatua za makusudi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa kutoa elimu juu ya uazi w mpangoili kukabiliana na ongezeko la idadi ya watu nchini.
Kwa upande wake Meneja Miradi ya Afya ya Mama na Mtoto kutoka Amref Health Africa Dkt.Sarafina Mkuwa alisema mradi huo utatekelezwa kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya mikitano mbalimbali itakayo wahusisha viongozi kuanzia ngazi za serikali mitaa pamoja na wananchi.

Aidha amewahakikishia wananchi kuwa matumizi ya njia za uzazi wa mpango hazina madhara kama baadhi ya watu wanavyopotosha,nakusema kuwa njia hizo ni salama.

Akitaja baadhi ya faida za uzazi wa mpango Dr. Mkuwa amesema kwamba inasaidia wakina mama kuwa na Afya bora,watoto kukua kwa mpangilio mzuri nakusaidia pia familia kuendelea kiuchimi.

No comments