Breaking News

Tanzania Kuwa Mwenyeji Wa Mkutano Wa Afrika Wa Bima Ya Maisha 2017

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mkutano wa Afrika wa Bima ya Maisha, Khamis Suleiman akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkutano habari

Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Kassim Majariwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kikao cha semina ya umoja wa makampuni ya bima afrika (AIC).

Akizungumza na waandishi wa habari Mapema leo jijini Dar es Salaam Mratibu wa Kamati ya maandalizi Bw. Khamisi Sulemani alisema semina hiyo itafanyika mjini Arusha katika ukumbi wa mikutano ya kimataifa (AICC).

Alisema semina hiyo inatarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia Novemba 1 hadi 3 hivyo wananachi wanataweza kuhudhuria fursa hiyo ili kutambua umuhumi wa  mwananchi kuwa bima.

Alisema  nchi za  Afrika bado kuna changamoto kwa wananchi kuhusu matumizi ya bima ambapo takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 0.7 ya wananchi wa Tanzania ndiyo wanaotumia bima, wakati nchini kenya asilimia 2.5, na Uganda asilimia 0.5.

“Swala la matumizi ya bima bado ni changmoto  hasa kwa nchi nyingi za afrika hivyo jitihada zaidi zinaitajika kuhakikisha wananachi wanapewa elimu juu ya faida ya matumizi ya mifuko hiyo” Alisema Bw. Sulemani.
Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya mkutano wa Afrika wa Bima ya Maisha, Magreth Ikongo akizungumza na waandishi wa habari.

Aidha Bw. Sulemani aliongeza kuwa “Kuna nchi zaidi ya 20 zitashiriki katika mkutano huu na mada zitakazozungumziwa ni pamoja na zile zitakazosaidia mwananchi mmoja mmoja na taifa kwa ujumla, kutakuwa na dama za bima kuangalia wapi tulipo na wapi tunapotaka kwenda,
“Azma yetu ni kuleta msisimko kwa wananchi husasi kwa wananchi kununua kiwango kikubwa cha bima kuliko ilivyo sasa hivi kwa kuongeza mteja mmoja mmoja na kuongeza mapato kwa taifa,” amesema Seleima.
Aidha Suleimani amesema mkutano huo utatumika kusaidia kukuza sekta ya utalii, “Tumeona hii ni fursa ya kipekee kuendeleza soko letu la utalii na ndiyo maana tumeamua kufanya mkutano huu Arusha na kutakuwa na siku moja ya kuwapa fursa wajumbe kuweza kutembelea vituo vya utalii.
Kwa upande wake mjumbe wa kamati ya maandalizi ya mkutano wa afrika wa bima ya maisha, Magreth Ikongo ametoa wito kwa makampuni yanayojihusisha na bima nchini kutumia fursa hiyo kutatua changamoto wanazoweza kumbana nazo.
Pia amewataka wananachi kujiokeza kwa wingi kuhudhuria kwenye semina hiyo ili luweza kujua dhana ya serikali kuwekwa msisitizo katika bima.

Semina hiyo ambayo imebeba kaulimbiu isemayo Mchango Sekta Ya Bima Katika Mapinduzi Ya Viwanda Na Maendeleo Endelevu.

No comments