Breaking News

Naibu Waziri Uchukuzi Na Mawasiliano Mhandisi Nditiye Waliojenga Makazi Katika Miundombinu Ya Reli Wavunje Nyumba Zao.

Naibu Waziri wa  ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye, akieleza jambo mbele ya baadhi ya viongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL)
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) Masanja Kadogosa akifafanua jambo mbele ya Naibu Waziri Atashasta Nditiye.


Wafanyakazi kutoka vitengo mbalimbali wakimsikiliza Naibu Waziri wa  ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye (hayupo pichani).

Dar es salaam:
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imewataka wananchi waliovamia na kujenga makazi  katika maeneo ya miundombinu ya Reli kubomoa nyumba zao kwa hiari yao kabla serikali  haijawasaidia kufanya hivyo.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Atashasta Nditiye alipotembelea Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) na kuelezwa kuwa imeanza kuboresha miundombinu kwa ajili ya kurejesha safari za treni kutoka Tanga kuelekea  Kilimanjaro hadi Arusha.

“Kwa hiyo wale ambao wamevamia maeneo ya reli wabomoe wengine, vinginevyo tutawasaidia na hata fidia ikibini ya kuwabomolea tutawadai,” amesema.

Aidha amesema kwa wale ambao walikuwa wamejenga kwa vibali harali na kufuatwa na miundombinu ya reli watalipwa fidia lakini kwa waliovamia hawatalipwa.

Amewataka wananchi katika maeneo yote nchini ambayo reli inapita kuhakikisha wanapisha ili ujenzi wa reli kwa kiwango cha Standard Gauge ufanyike bila vikwazo na kukamilika mapema.

Kwa upende mwingine amewataka watumishi wa TRL kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na taratibu za utumishi wa umma ili kuhakikisha wananchi wanahudumiwa vizuri kwa usafiri wa njia ya reli kwani atakayekwenda kinyume serikali haitamvumilia itamchukulia hatua za kisheria.

Akizungumzia kuhusu kuboreshwa kwa reli ya kutoka Tanga kuelekea Kilimanjao hadi Arusha, Mkurugenzi Mtendaji wa TRL Masanja Kadogosa, amesema maboresho hayo wameanzia Korogwa na sasa wamesakarabati kilometa 20  hadi Mombo na lengo ni kuanzia mwakani treni zianze safari kupitia reli hiyo.

Aidha amesema kinachowasukuma kufanya maboresho hayo ni kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya kiuchumi pamoja na kusafirisha abiria na mizigo nchini.

Akizungumzia ujenzi wa Reli ya Standard Gauge amesema hadi sasa maendeleo ya ujenzi huo ni mazuri na kwamba wamekwisha fanya usanifu na wemeanza ujenzi wa matuta pamoja na kambi.

Kwa upande wake Mkuu wa Operesheni wa TRL Focua Sahani amemweleza Naibu waziri kuwa Kampuni hiyo inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa wafanyakazi, wanahitaji vichwa visivyopungua 45 na kuboresha mabehewa 17.

No comments