Prof Mbarawa Akemea Vitendo Vya Rushwa Katika Miradi.
DAR ES
SALAAM:
Waziri
wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Profesa MAKAME MBARAWA ameiagiza
bodi ya usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji wa majenzi kuwafutia usajili
na kuwachukulia hatua kali wataalam wote watakaobainika kupokea au kutoa rushwa
katika kutekeleza wajibu wao.
Akizungumza
jijini Dar es salaam katika ufunguzi wa mkutano wa 28 wa wadau wa bodi ya
usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji wa majenzi amesema kuwa ni
muhimu kwa bodi kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika miradi ili kubaini wale
wote wanaukiuka taratibu kwaajili ya rushwa.
Waziri
MBARAWA ameipongeza bodi hiyo kukutanisha wataalam hao na wadau wa bodi
ya nchini Kenya na kuwataka kuendelea kukutana kubadilishana ujuzi na uzoefu kwakuwa
teknolojia inakua kwa kasi sana hivyo ni vema kujifunza zaidi ili kukabiliana
na majanga kama matetemeko ya ardhi.
Pia
ameipongeza bodi hiyo kwa kubuni michoro ya majengo kwa gharama nafuu na
kusema kuwa itawanufaisha watanzania katika kutatua matatizo ya ujenzi.
Aidha
Profesa MBARAWA ametoa agizo kwa wakurugenzi na watendaji wa masuala yanayohusu
ujenzi kuhakikisha vijana wanapewa fursa ya kuwekwa katika kila sehemu yenye
miradi mkubwa ili waweze kujifunza na kunufaika kupitia miradi hiyo.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa bodi ya usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji
majenzi ALBERT MUNUO amesema kuwa semina hiyo ni mwendelezo wa mpango wa
mafunzo endelevu ambazo bodi imekuwa ikiandaa kwa lengo la
kuwakutanisha wabunifu wa majengo,wakadiriaji majenzi na wataalam wanaohusiana
na sekta ya ujenzi lengo likiwa kujifunza mambo mapya yanayotokea katika
utendaji kazi.
Mkutano
huo wa bodi umewakutanisha wadau na wataalamu wa majenzi na makandarasi
mada kuu ni mbinu ya kupunguza madhara ya matetemeko ya ardhi,ukaguzi wa miradi
ya ujenzi na matengenezo ya majengo na miundombinu.
No comments