Mhe. Amina Shaban: Awataka Wahitimu Wa Chuo Cha PSPTB Kuacha Kupokea Rushwa.
Amina Khamis Shaaban
(aliyemwakilisha Dkt Ashatu Kijaji) akiongea na wahitimu wakati wa mahafari ya
chuo cha PSPTB yaliyofanyika viwanja
vya karimjee jijini dar es salaam
Kutoka
(kulia),Bw Ismail mwita ambaye ni mjumbe wa bodi wa PSPTB akiwa ni mmoja
wawaliopewa cheti kutokana na mgeni rasmi (wa tatu kutoka kulia) wakati wa mahafari ya chuo cha PSPTB yaliyofanyika viwanja vya karimjee jijini dar es salaam.
Wahitimu wa Ngazi ya
cheti cha msingi wapatao 23 ambao kwa pamoja wamesimama baada ya kutunukiwa wakati
wa mahafari ya chuo cha PSPTB yaliyofanyika viwanja vya karimjee jijini dar es salaam.
Wahitimu wa Ngazi ya cheti wapatao 280 wakiwa
wamesemama mara baada ya kutunukiwa wakati wa mahafari ya chuo
cha PSPTB yaliyofanyika viwanja vya karimjee
jijini dar es salaam
Ndugu na jamaa wa
wahitimu waliofika kuwasindikiza ndugu zao waliohitimu elimu ya ununuzi na
ugavi katika mahafari ya chuo cha PSPTB
yaliyofanyika viwanja vya karimjee jijini dar es salaam.
Picha
ya pamoja mgeni rasmi, Viongozi wa bodi na Wahitimu katika mahafali ya chuo cha PSPTB yaliyofanyika viwanja vya karimjee jijini dar es salaam.
Dar es salaam:
Wahitimu wa ngazi mbalimbali
katika fani ya manunuzi na ugavi wametakiwa kujiepusha vitendo vya kuomba na
kupokea rushwa pindi watekelezapo wajibu wao hili kusaidia serikali kuepuka
mzigo wa hasara kubwa ambayo imekuwa wakipata kufatia baadhi yao kujiusisha na
vitendo hivyo.
Akifungua sherehe za mahafari
hayo, mwenyekiti wa bodi ya ununuzi na ugavi Sr. Dkt. Hellen Bandiho alisema bodi itaendelea kusimamia na kukuza fani ya ununuzi na ugavi nchini ambapo
kati ya watahiniwa 3086 waliofanya mitihani, 1,101 wamefaulu.
"kutokana na mtaala wa bodi
kutambulika na kuthibitishwa na taasisi ya kimataifa ya IFPSM, wahitimubwa leo
wa ngazi ya CPSP watatunukiwa vyeti viwili, yaani cheti chetu cha CPSP na
cha IFPSM. Hii ni hatua kubwa katika kuwatambulisha wahitimu wetu katika soko
ajira kimataifa". Alisema Sr. Dkt. Hellen Bandiho
Pia ametanabaisha kuwa wakati
bodi hiyo uwapa miongozo ya maadili ya kitaaluma kwa kushirikiana na vyuo vya
mafunzo ya juu yameimizwa kuanzishwa kwa mafunzo mapya hali inayopelekea bodi
hiyo kutambulika kimataifa.
Aidha akizungumza katika mahafali
hayo Mgeni rasmi Dkt Ashantu Kijaji ambaye aliwakilishwa na Mhe. Amina Khamis
Shaban ameitaka bodi hiyo kusimamia mienendo ya wanataaluma ikiwemo kuchukua
hatua za kuwafutia usajili wale wote wanaokiuka taratibu na mienendo ya
taaluma.
“Ili
kuthibiti mienendo ya kimaadili ya wataalam wenu, ni lazima watu wote
wanaofanya kazi za ununuzi na ugfavi nchini, wawe wamesajiliwa na bodi kwa mujibu
wa sheria” alisema
Amina Shaban.
Pia amewahasa wahitimu kutumia
fulsa na utaalamu wao kwa manufaa ya taifa hili kusaidia kupunguza hasara ambayo
taifa limekuwa ikipata kutokana na ununuzi na ugavi, na kujiepusha wasitumie
fulsa ya elimu waliyopata kwa ajili ya kuchukua rushwa ili kufanikisha
ubadhirifu jambo litakalopelekea serikali kupata hasara.
Aliongeza kuwa “mtu yeyote atakayebainika kuingiza hasara
au kupokea rushwa kutokana na ofisi, cheo hama nafasi aliyonayo tutamfukuza na
kumfungulia mashitaka, serikali ya awamu ya tano haitamvumilia yeyote
atakayefanya kosa hilo”.
Hata hivyo amewataka
wahitimu hao kujiendeleza na wasibweteke kwa elimu waliyopata ila wanatakwia
kujiendeleza na kuwa wabunifu kutokana na mabadiriko ya teknolojia na
kimfumo yanayobadirika kila siku ili mambo mapya yasiwapite bila kujua.
No comments