Breaking News

JUKATA KUFANYA MAANDAMANO YA AMANI NCHI NZIMA KURUDISHA HAMASA YA WANANCHI KUSHIRIKI MICHAKATO YA KIDEMOKRASIA


Jukwaa la katiba Tanzania (JUKATA) limeadhamia kufanya maandamano ya amani nchi nzima yenye lengo la kurudisha hamasa kwa wananchi kuendelea kushiriki michakato ya kidemokrasia siku ya tarehe 30 mwezi huu ambapo ngazi ya kitaifa yatafanyika jijini Dar es salaam kuanzia ofisi za Jukata hadi viwanja vya Mnazi Mmoja.

Akisoma mbele ya waandishi wa habari mrejesho wa maadhimio ya kikao cha bodi na mkutano mkuu wa dharura uliofanyika tarehe 25 na 26 mwezi septemba katika ukumbi wa cathedral social hall mkoani Dodoma mwenyekiti wa JUKATA Bw Herbron Mwakagenda alisema tayali wameshamwandikia barua rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuomba ayapokee maadamano hayo.

Alisema sambamba na hitaji la kisheria pia Jukata wameshapeleka barua kwa jeshi la polisi kanda maalum ya dar es salaam, kwa upande ya mikoa mingine nje ya dar es salaam tayali pia wanachama wao wameshapeleka taarifa kwa wakuu wa polisi wa wilaya kuwafahamisha njia yatakapopita maandamano hayo ya amani na kuwaomba wakuu wa wilaya wa maeneo hayo kuyapokea.

“Maadhimio ya mkutano mkuu ambao wanachama wote 225 kutoka Tanzania bara na Visiwani na kutokana na maoni ya wananchi ambayo JUKATA imekuwa ikiyapokea tangu kutofanyika kura ya maoni kupitisha katika mpya mkutano huo kwa kauli moja wameadhimia kufanya maandamano ya amani nchi nzima hili kurudisha amasa kwa wananchi juu ya mchakato huo” Alisema Bw Mwakagenda.

Aidha Bw Mwakagenda aliongeza kuwa sambamba dhima ya maandamano hayo ametaja sababu kuu mbili ambazo JUKATA wameona ni vema maandano hayo yakapokelewa na Mhe Rais kuwa ni kutambua jitihada za Mhe Rais katika kusimamia rasilimali za madini, kupinga vita rushwa na matumizi mabaya ya mali za umma, kwa manufaa ya wananchi wa kizazi hiki na kijacho.

Alitaja sababu nyingine kuwa ni kufikisha kwa Mhe Rais ujumbe wa haja ya kurejewa kwa mchakato wa katiba mpya Tanzania ili ukamilike na kuwezesha kupatikana kwa katiba ya wananchi hivyo kusaidia hatua ambazo amekuwa akichukua kuweza yasilete tija na maendeleo endelevu ya muda mrefu kutokana na mengi kukosa msingi wa kkatiba.

Bw Mwakagenda pia ametoa wito kwa wandishi na vyombo vya habari wao kama nguzo muhimu katika jamii katika kufikisha habari na taarifa muhimu kwa taifa kuzipatia kipaumbele habari zinazohusu masuala ya kidemokrasia hasa suala la mchakato wa katiba mpya kwani kupitia wao wanaweza kujenga au kubomoa kwani taarifa ni moja ya silaha ambayo inaweza kuwa na madhara makubwa kama ikipotoshwa.


Vikao vya bodi na mkutano mkuu wa dharura ambao ulikutanisha wanachama wote 225 kutoka Tanzania na Zanzibar mjini Dodoma, Bw.Hebron Mwakagenda alichaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa  Jukwaa la katiba na Ndugu Mussa Kombo kutoka Zanzibar kuwa makamu Mwenyekiti kwa kipindi cha miaka mitatu.

No comments