Breaking News

Itel Mobile Yaadhimisha Miaka 10 Kwa Kuzindua Simu Mpya Za Kisasa Zaidi.


Makamu wa Rais wa Itel Mobile Bw.Leslie Ding akizungumza na wadau pamoja na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kuazimisha Miaka 10 ya Kampuni hiyo.

Kampuni ya Simu ya Itel Mobile imetimiza madhamisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwake huku ikiendelea kufanya vizuri katika soko la mauzo ya Simu na kuwa kinara kwa ubora wa bidhaa zake barani Afrika na nje ya Afrika.

Miaka 10 iliyopita Itel Mobile ilizindua mpango wa kumwezesha kila mmoja kuwa na simu bora kwa ajili ya mawasiliano ya uhakika,katika kipindi hicho chote tumepitia katika kipindi kigumu katika Nyanja za kiuchumi na kisiasa lakini tumeweza kufanikiwa kutimiza mlongo mmoja kwa uthabiti mkubwa.

Itel Mobile iliingia kwenye soko la Afrika mwaka 2007 na baada ya kuanzishwa kwa timu ya watu wenye ujuzi na moyo wa kufanya kazi na mpaka sasa miaka 10 kampuni hii imekuwa na kuweza kuenea zaidi ya nchi 45 Duniani kote.
Balozi wa Itel Mobile,Irene Uwoya akizungumza na wadau pamoja na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kuazimisha Miaka 10 ya Kampuni hiyo jijini Dar es salaam.

Ndani ya miaka 10 Itel Mobile imekuwa na mabadiliko makubwa chanya ya bidhaa kutokana na kufuatwa matakwa ya wateja wake hivyo imepelekea kupendwa na kuleta mvuto kutokana na kuboreshwa kwa bidhaa hizo kwa ubunifu mkubwa.

”Tumeweza kuongeza idadi ya wateja mara mbili zaidi barani Afrika na pia shukrani zetu za dhati ziende kwa wateja wetu pamoja na mashabiki wote wa Itel na mpaka sasa tumeuza jumla ya simu milioni 100’alisema Makamu Rais.

Aidha nguvu kubwa yetu inatokana na bidhaa zetu zilivyo bora pamoja na timu ya wafanyakazi wetu ambao kila mmoja amekuwa akijituma kutokana na nafasi yake na pia ubora na mvuto wa bidhaa unatokana na mapendekezo ya watumiaji wetu na huduma za matengenezo baada ya mauzo na warantii ya miezi 12 kwa bidhaa zetu zote.
MC Gara B kizungumza katika sherehe hiyo ya maadhimisho ya miaka 10 ya Itel Mobile Tangu kuazishwa kwake jijini Dar es salaam.
............
Hata hivyo tumekuwa na ushirikiano na mastaa wa nchi za Afrikia kama mabalozi wa kampuni yetu na wamekuwa kiungo muhimu katika kuleta ufahamu na uelewa kuhusu kampuni ya Itel ambapo imekuwa kampuni 3 bora barani Afrika.
Bw. Cooper Chein akielezea sifa na mafanikio ya simu ya Itel katika kipindi cha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake jijini dar es salaam.

Na kwa kuonesha upendo wetu Afrika tumekuwa tukifanya matendo ya ukarimu kwa jamii na kujitolea kutembelea baadhi ya shule na vituo vya watoto yatima kwa ajili ya kusaidia wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu.

Itel Mobile Tanzania kwa kushirikiana na balozi wa kampuni mwaka huu peke mpaka sasa tumewasaidia katika mahitaji muhimu zaidi ya watoto 400 wanaotoka mazingira magumu wakiwemo yatima na tunaendelea kuunga mkono jitahidi za kusaidia jamii.

Balozi wa Itel Mobile,Irene Uwoya akiwakabidhi Vyetina medani kwa baadhi ya wadau wao katika maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa Itel Mobile Jijini Dar es salaam. 

Wadau wakiangalia bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na Itel mobile katika maadhimisho ya miaka 10 ya tangu kuanzishwa Itel mobile jijini dar es salaam.

Tunaposherekea miaka 10 tunatarajia kuleta mabadiliko makubwa zaidi ili kuimarisha bara la Afrika kwa kutoa bidhaa bora za mawasiliano na leo tunazindua simu mpya ambazo ni za kisas zaidi yaani Itel S12 na S32 na zina ubora kutokana na kuwa kila  simu simu ina kamera mbili za mbele pia mwonekano mzuri na kusaidia kuchukua selfie ya kundi ambayo ina uwezo wa kuchukua watu wengi zaidi pia zina Fingerprint ‘alama za vidole’.



 Wasanii wakitumbuiza katika maadhimisho ya miaka 10 ya tangu kuanzishwa Itel mobile jijini dar es salaam.



Wadau wa kampuni ya Itel Mobile wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Itel Mobile katika maadhimisho ya miaka 10 ya tangu kuanzishwa Itel mobile jijini dar es salaam.


Wadau wakifatilia matukio mbalimbali katika maadhimisho ya miaka 10 ya tangu kuanzishwa Itel mobile jijini dar es salaam.

No comments