Breaking News

Kufatia Kuapishwa Wabunge 7 Wa Cuf Bungeni Jana Huu Ndio Msimamo Wa Kambi Ya Maalim Seif

Chama Cha Wananchi CUF Upande Unaomuunga Mkono Katibu Mkuu Wa Chama Hicho, Maalim SEIF SHARIF HAMAD Kimesema Hakiwatambui Wabunge Wanane Walioapishwa Jana Mkoani DODOMA.
Akizungumza Jijini Dar Es Salaam Kaimu Mkurugenzi Wa Habari wa CUF Bw.MBARARA MAHARAGANDE Alisema Kitendo Cha Kuapishwa Kwa Wafuasi Hao Kimefanyika  Haraka Bila Kuzingatia Utaratibu.
Alisema Michakato  wa Kuapishwa Kwa Wabunge Hao  Wapya ulipaswa Kusubiri Hatma Ya mashauri ya msingi yaliopo Mahakamani hivyo kumtaka Spika bunge mhe Job Ndugai Kujitathmini kutokana na unyeti wa nafasi yake ya kuongoza chombo hicho nyeti katika kutunga sheria na kuisimamia serikali kufatia kitendo cha kuwaapisha wabunge hao tayali Amepoteza Sifa kukiongoza chombe hicho.
Kwa upande wake Wakili wa chama cha CUF Bw. HASHIM MZIRAY Alibainisha kuwa Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Inaongozwa Na Katiba Hivyo Maamuzi Ya Kuondolewa Yanaweza Kukatiwa Rufaa.
Akizungumza kwa niaba ya Wabunge Waliovuliwa Uanachama Bi.RIZIKI SHAHARI Alisema Wataendelea Kupigania  Demokrasia Na Kuzitaka Taasisi Za Serikali kuacha kuingilia mambo ya ndan ya vyama vya siasa pamoja na kutumika Kuhujumu Vyama Vya Upinzani.

Chama Cha Wananchi (CUF) Kimekuwapo Katika Mgogoro Wa Muda Mrefu kati ya Katibu Mkuu Maalim SEIF SHARIF HAMAD Na Profesa IBRAHIM LIPUMBA Ambao Umesababisha Kufunguliwa Kwa Mashauri Mbalimbali Yanayoendelea Mahakamani kuu jijini dar es salaam.

No comments