Breaking News

Bonanza La Michezo Chuo Cha Kitm Lafana Jijini Dar

Meneja wa Benki ya NMB Bi. Janeth Shango ambae ndiye mgeni rasmi akizungumza wakati wa ufunguzi wa bonanza la michezo lililondalia na chuo cha Kilimanjaro institute of Technology andabusiness Management katika viwanja vya shule ya mapambano jijini Dar es salaam. 
Rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo hicho bw. Fredrick Semiono akifafanua jambo katika ufunguzi wa bonanza la michezo lililondalia na chuo cha Kilimanjaro institute of Technology andabusiness Management katika viwanja vya shule ya mapambano jijini Dar es salaam.
Waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi wa chuo cha Kilimanjaro institute of Technology andabusiness Management Bw. hilal alum akimkaribisha mgeni rasmi katika ufunguzi wa bonanza la michezo lililondalia na chuo cha Kilimanjaro institute of Technology andabusiness Management katika viwanja vya shule ya mapambano jijini Dar es salaam.

Mgeni rasmi Meneja wa Benki ya NMB Bi. Janeth Shango akikagua timu za mpira wa miguu tayali kwa kuanza kwa mchezo kati ya wanafunzi na walimu wa chuo hicho.

Dar es salaam
Wito umetolewa kwa wanafunzi wanaosoma katika vyuo mbalimbali nchini kutoa kipaumbele katika maswala ya michezo pamoja na kuwa ni burudani pia michezo ni afya pamoja na nyenzo muhimu katika kuwafanya wanafunzi hao kufatilia masomo yao.

Akizungumza wakati ufunguzi wa bonanza la michezo la wanafunzi wa chuo cha kilimanjalo Institute of Technology jijini dar es salaam, Meneja wa Benki ya NMB Bi. Janeth Shango alisema michezo ni afya pia michezo burudani hivyo kuwataka wanafunzi wa vyuo vikuu kuendelea kutenga mda wao baada ya ratiba za masomo kwa ajili ya kushiriki katika michezo.

Alisema benk ya NMB kwa kutambua umuhimu wa michezo wameona ni jambo jema kujumuika katika bonanza hilo kwani wanafunzi ambao wanajihusha na maswala ya michezo mara nyingi wanakuwa ni watu wenye furaha na wenye afya nzuri na kuzuia magonjwa.

Bi Shango Aliongeza kuwa kupitia bonanza hilo ambapo michezo mbalimbali itachezwa na kuwakutanisha wanafunzi na walimu wa chuo hicho katika michezo mbalimbali inaonyesha namna chuo hicho kilivyo na mahusino mazuri kati ya wananfunzi na walimu.

Kwa upande wake Rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo hicho bw. Fredrick Semiono alisema lengo kubwa la kuandaa bonanza hilo nikuwakutanisha wanafunzi na walimu wa chuo hicho katika kushiriki michezo sambamba na kuboresha mahusiano kati yao kupitia michezo.

Alisema jumla ya timu nne kutoka katika fani mbalimbali zitachuana vikali katika michezo ya mpira wa miguu ambapo fainali ya itafanyika siku ya terehe 9 mwezi huu katika fukwe za Hoteli ya Jangwani sea Breez jijini dare s salaam na washindi kukabidhiwa zawadi zao.

Amezita timu ambazo zinashiriki katika bonanza hilo kuwa ni timu ya Accounting, Information Technoloy, Diploma Of Bussiness manegment na Diploma of PS ambapo shindig wa kwanza katika mashindano hayo atajinyakulia fedha taslimu pamoja na kiroba cha mchele.

No comments