Breaking News

Mhe Masauni Awataka Wanafuzi Wanaosoma Masomo Ya Uhandisi Kuongeza Ubunifu Zaidi

Related image
Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Hamad Masauni ametoa wito kwa wanafuzi wanaosoma masomo ya uhandisi kuongeza ubunifu zaidi ili kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa viwanda.

Mhe. Hamad Masauni ametoa wito huo wakati wa ufunguzi wa   maonesho ya pili ya miradi mbalimbali iliyofanywa na wanafuzi wa Chuo kikuu cha Mtakatifu Joseph, kilichopo Mbezi jijini dare s salaam.

Alisema wanafuzi wanatakiwa kuhakikisha wnawekeza katika swala la ubunifu ili nchi iweze kuwa na wabunifu wakutosha hususani katika zama hizi za sayansi na teknolojia jambo ambalo litakuwa chachu ya maendeleo.

“Katika Taifa lolote duniani Serikali imekuwa inawategemea vijana  wasomi katika fani mbalimbali hususani uhandisi kuleta mapinduzi kiuchumi pamoja viwanda ili nchi iweze kwenda iweze kusonga wabunifu wanahitajika .”alisema Masauni.

Alisema katika siku za hivi karibuni kumekuwa na Shule nyingi ambazo zinafundisha kozi mbalimbali za kihandisi tofauti na miaka ya zamani ambapo  Vyuo vilikuwa vichache.

Serikali haitakuwa nyuma kuwasaidia wanafunzi wabunifu wanatakao buni vitu mbalimbali ambavyo vitalisaidia Taifa kuleta  maendeleo ya haraka hususani katika Viwanda.

“Nawaombeni wanafuzi kuwa na imani na Serikali ya awamu ya tano  ongezeni taaluma zaidi katika masomo yenu vijana ndiyo nguvu kazi.” alisema Masauni.

Kwa uapnde wake Makamu mkuu wa Chuo wachuo cha st Josoph, Bw. Bhaskara Raju  alisema wanafuzi hao wameweza kubuni mashine mbali mbali ikiwemo Gari lisilo tumia mafuta pamoja na mashine ya kumenyea nazi ambapo zita wasaidia wanafunzi wenyewe kujiajiri.

“Wakati serikali inakwenda kasi kwa sera ya viwanda na wanafuzi wetu wamakuwa mstari wa mbele kuweza kulitangaza taifa lwa kubuni vitu ambavyo vitaweza kuleta mabaliliko.” alisema Raju

Aidha Bw. Raju aliongeza kuwa maonesho hayo yamekuwa yakiwasaidia wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali pamoja na wanafuzi wa sekondari kujifunza na kuona ubunifu unaofanywa wezao.

Naye Mmoja wa wanafuzi wa Chuo hicho Meshack Zephania aliyetengeneza gari linalotumia umeme wa jua alisema aliweza kuangalia mfumo wa gari ndipo  naye akatengeneza.

“Mimi nilikuwa na mawazo ya kutengezeza gari lakinio nilipo kaa na kuingia darasani kupatiwa mafunzo na walimu niliweza kuunda kifaa hicho”. Alisema Zephania.

Pia aliwaomba wanafuzi wa masomo uhandisi chini  kuacha kukaa na mawazo yao kichwani bali waweze kuyatendea kazi lilikukuza taifa kiuchumi

Kwa upande wake Bi Sophia Abeld anayesoma chuoni hapo mwaka wa mwisho alisema Taifa likiwa na vijana wanaokuwa na uwezo wakutengeneza vifaa mbalimbali za kiubunifu kama ya kupandia mahindi wa watapunguza tatizo la ajira nchini.