Breaking News

Kanisa La EAGT Lamwomba Rais Kuingilia kati Mgogoro Wa Kiwanja Uliodumu Zaidi Ya Miaka 30.

Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Temeke limemuomba Rais Dkt John Pombe Magufuli kuingilia mgogoro wa umiliki wa kiwanja kilichopo kitalu D mtaa wa Everest uliodumu zaidi ya miaka 30.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam Mdhamini wa Kanisa la EAGT nchini Mchungaji Christom Isack Ngowi alisema kufuatia notisi inayowataka kuhamisha mali zote za kanisa kabla ya kesho Agosti 21, siku ambayo Manispaa ya Temeke imepanga kubomoa eneo hilo, kitendo ambacho waumini na viongozi wa kanisa hilo wamesema kingesubiri maamuzi ya barua waliyomuandikia Rais Magufuli kuhusu mgogoro huo.
Alisema  eneo hilo ambalo kanisa lilianza kuomba umiliki wake tangu mwaka 1978 viongozi na waumini wa kanisa hilo wameshangazwa na kile walichoeleza kuwa ni kutotekelezwa kwa maagizo ya mawaziri wa zamani wa ardhi akiwemo marehemu Mustafa Nyang'anyi na mwenzake Marcel Bujiku Komanya, ambao katika nyakati tofauti walizitaka mamlaka kulipatia kanisa la EAGT Temeke umiliki wa eneo hilo.

“Vingozi wa kanisa pamoja na kuchukua hatua mbalimbali kuwasiliana na mamlaka husika kumekuwepo na sintofahamu kuhusu umiliki wake hivyo tumemwandikia barua mhe Rais Magufuli juu ya mgogoro huu kwani ndio mtu pekee ambae anaweza kusimamia haki ambayo tumekuwa tukifatilia kwa zaidi ya miaka 30” Alisema Mchungaji Ngowi.
Mgogoro wa Kiwanja hicho uliibuka kufatia mfanyabiashara mmoja wa eneo hilo kudai ndio mmiliki wa eneo hilo tangu mwaka 1999.

No comments