Breaking News

Dc Wa Ubungo Kisale Makori Amaliza Mgomo Wa Madereva Kituo Cha Simu 2000.

Mkuu wa wilaya ya ubungo Mhe Kisale Makori ameutaka uongozi wa kituo cha mabasi cha simu 2000 kusitisha ongezeko la tozo ambalo linawataka madereva wanaotumia kituo hicho kulipa la shilling 1000 na badala yake waendelee kutoza shilingi 500 kama ilivyokuwa awali.

Kauli hiyo inakuja mara baada ya madereva wanaotumia kituo hicho cha simu 2000 kugoma kutoa huduma za usafiri kufatia kualalamikia ongezeko hilo ambalo wamedai aliendani na hali halisi ya kituo hicho pamoja na kutoshirikishwa katika mchakato mzima wa kuandaliwa kwake.

“Naagiza kusitishwa kwa mda tozo mpya ya shilingi 1000 na iendelee kutumia ya awali ya shilingi 500 na namwagiza mkurugenzi wa manispaa ya ubungo, meneja wa kituo pamoja na viongozi wa madereva kukaa kujadiliana juu ya hili swala kwani kwa mujibu  wa madai ya madereva yana hoja za msingi. Alisema mhe Makori.
Mapema wakizungumza kituoni hapo baadhi ya madereva walisema wameamua kugoma kufatia uongozi wa kituo hicho kuongeza ushuru kutoa shilingi 500 hadi 1000 bila kuangalia hali halisi ya biashara pamoja na changamoto nyingi zilizopo kituoni hapo.

“Uongozi wa kituo hicho umeamua kupandisha ushru japo tayali unajua changamoto zilizopo kituoni hapo ambazo tayalitulishaziainisha katika barua yetu kwa uongozi lakini chakushangaza uongozi wa kituo hicho umekuwa wakishindwa zipatia ufumbuzi matokeo yake wamekuja na ongezeko la bei ya ushuru kituoni hapo”  Walisema 
Wamezitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na obovu wa barabara inayotumika kuingia na kutoka kituoni hapo pamoja kuwepo na malalamiko kutoka kwa abiria ambao wanatumia kituo hicho hasa nyakati za usiku kufati miundombinu ya taa kituoni hapo kutofanya kazi hivyo kuofia usalama wao.


Alisema changamoto nyingne ni kuwepo na utaratibu mbovu kwa wakusanya ushuru wa kituo hicho jambo ambalo limekuwa kero na usumbufu kwa kipindi kirefu kwa madereva wanaotumia kituokutokana na tabia zao za kuwatishia pamoja na kutorudisha chenji pale wanapolipwa hela ya ushuru na kutakiwa kurudisha chenji.

No comments