WANAWAKE WEKENI MKAZO KATIKA MALEZI BORA ILI KUWA NA TAIFA BORA NA LENYE MAADILI.
Wito
umetolewa kwa Watanzania kulinda amani tuliyonayo na kudumisha maadili katika
jamii ili kuwa na Taifa bora na lenye maendeleo.
Akizungumza
kwa Niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan wakati wa ufunguzi wa kongamano kubwa la siku tatu la kuombea
Taifa Naibu waziri Elimu, sayansi, Tekinolojia na Ufundi Injinia Stella
Manyanya alisema wananwake ndio wenye jukumu kubwa la kuhakikisha wanatilia
mkazo katika swala la malezi bora jambo litakalopelekea taifa linakuwa bora .
Alisema
hili kuwa na kuwa na taifa bora na lenye maendeleo chanya mkazo zaidi
unaitajika kwa walezi kwa kuwalea vijana katika misingi bora ni jukumu la
wanawake hivyo kupitia kongamano hilo litawasasaidia kuwajegea uwelewa washirki
kutambua wajibu wao katika familia.
Aidha
amewataka watanzania kumuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Dk.John Pombe
Magufuli na serikali yake ya awamu ya tano kwa hatua anazochukua kuleta
maendeleo sambamba na kupigania haki za wanyonge na masikini.
Kwa upande wake Mratibu
wa Kongamano la wanawake waombolezao kwajili ya Taifa Mchungaji Deborah
Godfrey Malassy alisema watanzania tuna kila sababu ya kujivunia kumpata Rais
muadilifu, mchapakazi na mwenye kupigania rasilimalia za nchi ambazo zimekuwa
zikipotea na kukosesha haki za wanyonge hapa nchini.
Alisema rais
Magufuli ni tunu kwa taifa kwani taifa limekuwa likipoteza asilimali zake lakini
kwa hatua ambazo ameanza chukua rais Magufuli inaonyeshakuzaa matunda hivyo
kuwataka watanzania wote kila mmoja kwa imani yake kumwombea rais hili aendelee
kutekeleza majukumu yake.
Nae Mchungaji Emanuela Mtafikilo akiwasilisha mada
katika kongamano hilo alisema jukumu la kila mzazi kulinda maadili kwa watoto
na kutenga muda wa kukaa na watoto wao hili kujua tabia za watoto kwani
jambo hilo linajenga upendo.
Alisema
kumekuwa na tabia za wazazi kuwaachia watoto wakitumia mitandao ya
kijamii na kuangalia vipindi vya luninga wakati wote jambo ambalo linapelekea
kuwepo mmomonyoko kubwa wa kimaadili.
No comments