Breaking News

PICHA:WAZIRI MAHIGA AFUNGUA MKUTANO WA 19 WA WAJUMBE WA KAMATI YA MAWAZIRI WA NCHI ZA JUMUIYA YA MAENDELEO KUSINI MWA AFRIKA (SADC).

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Mawaziri wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (hawapo pichani) wakati akifungua mkutano wa 19 wa kamati hiyo unaojadili ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Dr. Stergomena L. Tax akitoa neno la utangulizi wakati wa mkutano wa 19 wa Kamati ya Mawaziri wa nchi za jumuiya hiyo inayojadili ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Mawaziri wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (hayupo pichani) wakati akifungua mkutano wa 19 wa kamati hiyo unaojadili ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama mapema hii leo jijini Dar es Salaam.

No comments