Breaking News

MAKAMU WA RAIS MHE SAMIA MGENI RASMI KESHO KATIKA KONGAMANO KUBWA LA AINA YAKE LA WANAWAKE WAOMBOLEZAO KITAIFA


DAR ES SALAAM:
Makamu wa rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kesho anatajiwa kufungua Kongamano kubwa la aina yake la wanawake waombolezao kitaifa kwaajili ya kuliombea Taifa litakalofanyika kwa muda wa siku tatu. 

Akizungumza mapema leo jijini Dar es salaam na Mratibu wa kongamano hilo Mchungaji Deborah Godfrey Malasy alisema lengo kuu la kongamano hilo ni kuwakutanisha wanawake kutoka madhehebu mbalimbali nchini hili kuwajengea uwezo kutambua nafasi yao katika jamii.
Alisema  kupitia kongamano hilo wakimama ambao ni viongozi kuwafundisha  kutambua nafasi zao katika jamii hili wawe majasiri  katika kuongoza wengine kujiepusha na unyanyasaji wa kijinsia ili waweze  kuitumia fursa ya uongozi walizonazo hili kujikwamua  kiuchumi

Aidha Mchungaji Debora aliongeza  kuwa Maudhui ya Kongamano ni "Tanzania Mpya"ambapo  watafanya maombi maalum kwajili ya kuombea vijana ili kurejesha maadili ambayo kwasasa yameporomoka ambapo neno la Mungu litakuwa kutoka Yeremia  tisa  17 hadi 21.

Pia Mchungaji Debora ametoa kwa serikali ya awamu ya inayoongozwa na Rais Dk.John Pombe Magufuli kwa kuwa muadilifu, mchapakazi na mwenye kujali wananchi wake kwakuwa ndiye kiongozi waliyekuwa wakimuomba Mungu awapatie.

Kongamano hilo la siku mbili linatarajiwa  kuanza kesho na kumalizika tarehe 22 Julai linakutanisha wanawake wa madhehebu mbambali kutoka ndani na nje ya nchi


No comments