NYANI AZIMA UMEME KWA ZAIDI YA SAA 6 ZAMBIA
Nyani
azima umeme kwa karibu saa 6 nchini Zamabia
Nyani
alivuruga mitambo ya umeme katika mji wa Livingstone nchini Zambia na kukata
umeme kwa karibu watu 50,000.
Nyani huyo
alifanikiwa kuingia katika kituo cha umeme siku ya Jumapili, na kuvuruga
mitambo yenye umeme inayosambaza umeme kuenda maeneo ya Kusini na magharibi mwa
Zambia kwa mujibu wa kampuni ya umeme nchini humo Zesco.
Alisema kuwa
wakaazi 28,000 wa Livingstone na watu wengine 22,000 wa eneo hilo walibaki
kabisa bila umeme kwa zaidi ya saa sita wakati ukarabati ulikuwa ukiendelea.
"Nyani
huyo alipigwa na umeme lakini kutokana na maumbile yake ya kimazingira alipata
tu majeraha mabaya ya moto. Kama angekuwa binadamu angekufa." alisema
Kapata.
Kapata alisema
kuwa kampuni hiyo imeomba msamaha wateja wake kwa hasara waliyoipata.
Mji wa
Livingstone ni maarugu kwa wanyama pori kama nyani na ndovu wanaotoka mbuga
iliyo karibu.
No comments