Breaking News

TGNP YATOA MAFUNZO KWA ASASI ZA KIRAIA KUHUSU MIKATABA YA MALENGO ENDELEVU YA KITAIFA NA KIMATAIFA YA KIJINSIA .

jioneee tgnp.Still003
Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) Imeandaa warsha ya mafunzo kwa asasi mbalimbali za kiraia na wadau wa serikalni ili kujadili mchakato wa mikataba ya  malengo endelevu ya kitaifa na kimataifa ya kijinsia .

Akizungumza jijini Dar es saalam Mkurugenzi mtendaji wa TGNP mtandao Bi.Lilian Liundi amesema kuwa lengo ni kuangalia mikataba hiyo kama imekidhi mfumo wa kuondoa ukandamizi dhidi ya wanawake katika kuleta maendeleo katika sekta ya maji,afya na elimu na nafasi za uwiano  katika  uongozi baina ya mwanamke na mwanaume.


Bi. Liundi amebainisha kuwa katika kuhakikisha maendeleo endelevu yanakuwepo ni vema kwa wanaume kukubali kuwa sehemu ya mabadiliko kwa kinamama ili kuweza kufikia malengo ya kimaendeleo ifikapo mwaka 2030.
jioneee tgnp.Still002
Aidha amesema kuwa katika masuala muhimu yanayojadiliwa ni pamoja na kuangalia bajeti zinazosomwa endapo zimezingatia vigezo vya kuondokana na uonevu kwa wanawake kama ndoa za utotoni,ukatili wa kijinsia na usawa wa madaraka baina ya mwanamke na mwanaume.

Amesema kuwa ni vema serikali  na vyama vya siasa nchini kutoa kipaumbele kwa wasiojiweza  na walemavu
Nae  mshauri na mtaalam wa masuala ya jinsia wa TGNP mtandao Bw. Edward Mhina amesema kuwa taswira inayotakiwa kufikia mwaka 2030 hedhi  kwa watoto wa kike isiwe kizuizi au sababu ya kukosa masomo.

Ameongeza kuwa ni vema watoto wa kike na kiume kupata elimu ya msingi hadi chuo kikuu kwa usawa pasipo ubaguzi wowote.
Amesema  kuwa wanawake wamekuwa wakibeba mizigo kwa makadirio ya tani tano kwa mwaka jambo ambalo kwa kuliangalia ni uonevu na kandamizi kimfumo baina ya kike na kiume.

Mbali na hayo amesema kuwa kuna haja ya kuangalia viashiria  ili kuweza kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa Tanzania ya viwanda ili kukuza uchumi na kuleta maendeleo baina ya jinsia.
Mafunzo hayo ya siku tatu yameandaliwa na TGNP na kushirikisha wadau mbalimbali na asasi zisizo za kiserikali yamelenga kuangalia mchakato wa mikataba ya kimataifa ya kijinsia katika kuleta maendeleo.

No comments