Breaking News

RAHCO YAWATAKA WALIOJENGA PEMBENI YA NJIA YA TRENI KUVUNJA NYUMBA ZAO MARA MOJA

Kaimu Mkurugenzi wa RAHCO, Bw Masanja Kadogosa akizungumza na waandishi wa habari 


 Kaimu Mkurugenzi wa RAHCO, Bw Masanja Kadogosa akikagua eneo hilo

Dar es salaam
Kampuni hodhi ya rasilimali za Reli (RAHCO) imewataka wananchi wote waliojenga ndani ya eneo la mradi wa Reli na wale waliowekewa alama za X kuvunja nyumba hizo mara moja.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) Bw.Masanja Kadogosa kuwa serikali imewataka wananchi  kutekeleza jukumu la kuvunja hizo kwakuwa muda  walopewa ni wa kutosha.

Kadogosa alisema kuwa kwa mujibu wa sheria  ni kosa kwa wananchi wote waliojenga ndani ya mita 30 katika eneo la reli wavunje haraka ili kupisha mradi wa ujenzi wa Reli ya kisasa ya Standard Gage.

Ameongeza kusema kuwa ujenzi  huo tayari serikali kupitia RAHCO imefanya malipo ya awali kwa mujibu wa mkataba ili ujenzi huo uanze mara moja.

Amebainisha kuwa hatua mbalimbali za ujenzi wa mradi zimeshaanza usanifu jenga kwaajili ya kambi tatu za kufanyia kazi ambazo zimejengwa katika maeneo ya Ilala-Shaurimoyo Dar es salaam, Soga-Kibaha na Ngerengere iliyopo Morogoro.

Pamoja na hayo Bw.Kadogosa amesema katika kuhakikisha unakamilika kwa wakati Rahco imekabidhi magari nane kwa mshauri mwelekezi anbaye anasimamia mradi huo ili ukamilike kwa wakati.

Aidha amesisitza kuhusu kampuni za wazawa ambazo zinahitaji tenda mbalimbali katika mradi huo kuwa tayari wapo katika hatua za mwisho za kufungua website itakayotumika katika kutoa na kuchapisha taarifa na tenda zote za mradi na kusema hakutakuwa na upendeleo katika tenda.


No comments