Breaking News

ITEL MOBILE YATOA MKONO WA SIKUKUU YA EID AL FITR KWA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA JIJINI DAR

Balozi wa Simu ya ITEL Bi Irene Uwoya akimkabidhi katibu mtendaji wa kituo cha kulelea watoto cha CHAKUWAMA bwana Hasan Khamis msaada wa mchele, unga, sukali, mafuta ya kula na vifaa mbalimbali vya shule kwa niaba ya watoto wa kituo hicho.





Balozi wa Simu ya ITEL Bi Irene Uwoya akitoa zawadi kwa watoto wanaoishi katika kituo cha kulelea watoto cha CHAKUWAMA jijini dare s salaam
katibu mtendaji wakituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu bwana Hasan Khamis akizungumza mara baada ya kupokea msaada mapema jijini dar es salaam


Balozi wa Simu ya ITEL Bi Irene Uwoya akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutoa msaada mapema leo jijini Dar es salaam.

Dar es salaam
Kampuni ya itel mobile kupitia kwa balozi wake nchini msanii wa maigizo ( Bongo movie) Bi Irene Uwoya leo imetoa msaada kwa kituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu cha CHAKUWA kilichopo sinza jijini dar hili kuweza kusherekea vizuri sikukuu ya Eid Al Fitr.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo jijini dar es salaam mkurugenzi wa ITEL Bw, Saphon Asajile alisema wanaunga mkono jitihada zinazofanywa na kituo hicho pamoja na vingine ambavyo vimekuwa vikihakikisha watoto wanakuwa na furaha pamoja na kupata mahitaji yanayostahili.

Alisema kwa kutambua tupo katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na hiki ni kipindi cha maandalizi ya kuelekea sikukuu ya Eid Al Fitr, wametoa msaada wa Mchele kg 100, Mafuta ya Kula lita 30, Sukari, Unga wa sembe kg 25 pamoja na vifaa vya shule madaftari 200 na kalamu  100 hili na wao waweze kusherekea kwa furaha kama watoto wengine.

Bw. Asajile aliongeza kuwa msaada huo unatokana na ushirikiano mzuri uliopo kati ya wateja wao na kampuni hiyo sambamba na kutoa wito kwa jamii kuonyesha upendo kwa watoto waishio katika mazingira magumu nchini pamoja na kuendelea kununua simu za ITEL.


Kwa upande wake katibu mtendaji wakituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu bwana Hasan Khamis ameishukuru kampuni ya ITEL pamoja na Balozi wake Irene Uwoya kwa msaada huo kwani umekuja mda muhafaka na sahihi kwao na kuwataka kuendelea na moyo kwa kuendelea kusaidia makundi yasiyojiweza.

No comments