Breaking News

WATANZANIA KUFANYA MIAMALA YA KIFEDHA KUPITIA HALOPESA NA NMB

Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Halotel, Bw. Le Van Dai akisaini mikataba wakati wa tukio hilo. Kulia niKaimu Mkuu wa Huduma Binafsi za Kibenki wa NMB, Boma Raballa akisaini tukio hilo 
Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Halotel, Bw. Le Van Dai akizungumza katika tukio hilo la huduma ya Halopesa juu ya kuunganishwa na benki ya NMB.  Kushoto ni  Henry Mavulla Mwendesha Biashara wa Halopesa na kulia ni Kaimu Mkuu wa Huduma Binafsi za Kibenki wa NMB, Boma Raballa. 

Kaimu Mkuu wa Huduma Binafsi za Kibenki wa NMB, Boma Raballa akizungumza juu ya tukio hilo. kushoto ni Henry Mavulla Mwendesha Biashara wa Halopesa na katikati ni Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Halotel, Bw. Le Van Dai.

Kaimu Mkuu wa Huduma Binafsi za Kibenki wa NMB, Boma Raballa akibadilishana nyaraka wakati wa tukio hilo na Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Halotel, Bw. Le Van Dai

Na Frank wandiba
Katika kuakikisha wanapanua wingo wa huduma za kifedha kwa wananchi wenye kipato cha chini Kampuni ya mawasiliano  ya Halotel kwa kushirikiana na benki ya Nmb  wamezindua huduma ya kufanya mihamala ya kifedha kupitia halopesa hili kuwawezesha watanzania kunufaika na huduma za kifedha nchi nzima

Akizunguumza katika halfa ya uzinduzi huo mapema leo jijini dar es salaam Naibu Mkurugenzi wa kampuni ya Halotel Bwana Le Van Dai alisema ushirikiano huu wa kipekee ambao umelenga katika kurahisisha maisha ya watanzania hasa waishio vijijini anbao wamekuwa wakipata tabu kupata huduma za kifedha kutokana na maeneo wanayoishi.

“Tuanatambua changamoto ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa kikwazo kwa wananchi wengi hasa wa kipato cha chini kutokana na wengi wao kukwama kuweza kupata huduma za kifedha kutokana na miundombinu kutowafikia katika maeneo yao” alisema bw Dai.

Pia bwana Dai aliongeza kuwa azma  ya serikali ni  kuzitaka taasisi zote zinazojihusisha na fedha kuwafikia wananchi wote hasa wa maeneo ya vijijini na kusema kuwa huduma hiyo itapunguza kadhia kwa watumishi wa umma na sekta nyinginezo anbako huduma za kibenk azijafika.

Alisema kupitia mawakala wake zaidi ya elfu 30  nchi nzima huduma hii itawasaidia kuwawezesha wakazi hususani wanaoishi katika maeneo ambayo hayakuwahikuwa na mawasiliano au huduma za kibenkisasa kuweza kuweza kupata huduma za kifedha kuotia simu za mkononi.

Kwa upande wake Kaimu wa huduma Binafsi za kibenki wa NMB bw Boma Rabala alisema ushirikiano huu ni moja ya mafanikio mengne makubwa ya kibishara kwao hususani katika kupanua wingo wa utoaji wa huduma zake sambamba na kuwawezesha watanzania wengi zaidi kupata huduma za kifedha popote walipo.

Alisema kupitia ushirikiano na kampuni ya mawasiliano ya  halotel wana amini wataweza kufikia lengo la serikali na benki hiyo kuweza kuwafikia wateja wengi zaidi.

Bw  Rabala aliongeza ushirikiano huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kurahisisha na kuboresha hali ya maisha na uchumi wa watanzania.

No comments