Breaking News

EWURA YATANGAZA BEI MPYA YA MAFUTA ZITAKAZOANZA KUTUMIKA NCHINI KESHO.


Image result for picha ya mkurugenzi wa ewura
MAMLAKA ya Udhibiti huduma za nishati na majini nchini (ewura) imetangaza bei mpya ya mafuta Petrol, dizeli na mafuta ya taa ambayo itaanza kutumika kuanzia tarehe 4 mwezi januari mwaka 2017.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari na kusainiwa na mkurugenzi mkuu  wa EWURA Bwana Felix Ngamlagosi inaonyesha kuwepo na mabadiliko ya bei kwa mafuta ya aina zote ukilinganisha na toleo la bei  la mwaka jana desemba 07. 2016.


Taarifa hiyo inaonyesha kuwa bei ya rejereja kwa dizeli na mafuta ya taa mwezi januari 2017 itapungua kwa Tsh 66 kwa lita sawa na asilimia 3.68, kwa upande wa petrol bei imeongezeka kidogo kwa shs 0.10 kwa lita sawa na aslimia 0.01 ukilinganisha na teleo la bei za mwaka jana.
Image result for ewura logo
Kwa upande wa bei za jumla kwa mafuta ya dizeli na mafuta ya taa zimepungua nazo kwa Tshs 66 kwa lita sawa na asilimia 3.91 na Tsh 37 kwa lita sawa na asilimia 2.25, kwa upande wa Petroli bei imeongezeka kidogo Tsh 0.01kwa lita sawa na asilimia 0.01.

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa hakutakuwa na mabadiliko ya bei ya mafuta kwa mkoa wa Tanga hii ni kutokana na kutokwepo na shehena mpya ya mafuta kwenye bandari ya Tanga tangu mwezi desemba 2016 hivyo kupelekea bei ya mafuta mkoa huo kwa mwezi januari kubaki kama  ilivyokuwa mwezi wa desemba 2016.

Pia taarifa hiyo imebainisha kuwa mabadiliko ya bei ya mafuta ya reja reja katika mkoa wa Dar Es Salaam Petrol 1890, Diseli 1732 wakati mafuta ya taa itakuwa 1700, mabadiloko ya bei za mafuta nchini yanatokana na mabadiliko ya soko la mafuta duniani.

No comments