Breaking News

SERIKALI YA MISRI YAMKAMATA MWANAHABARI WA AL-JAZEERA


Serikali ya Misri imedhibitisha kwamba inamzuia mwanahabari kutoka shirika la habari la AlJazeera aliyekamatwa Ijumaa.

Wizara ya usalama wa ndani inasema mwanahabari huyo, Mahmoud Hussein, atazuiliwa kwa kipindi cha siku 15 kwa tuhuma za kuchochea maasi na kusambaza habari za uongo.

Television ya Al Jazeera ambayo imepigwa marufuku kuendesha shughuli zake nchini Misri,  imelaani hatua hiyo ya kukamatwa na kwa mwandishi huyo.

Kulingana na Aljazeera, mwanahabari huyo raia wa Misri alikuwa nchini humo kwa ajili ya likizo.


Aljazeera television katika taarifa yake imesema inahofia usalama wa mwanahabari huyo.

                                                    chanzo Bbc

No comments