Breaking News

MUFTI MKUU SHEIKH DKT. ABUBAKAR ZUBER ATOA VYETI KWA WADAU WALIOFANIKISHA TAMASHA KUBWA LA KIMATAIFA KUHIFADHI QUAN KWA WANAWAKE

Mufti mkuu wa Tanzania sheikh Dokta Abubakar Zuber Bin Ally ametoa vyeti vya shukrani kwa kutambua mchango wa taasisi na wadau mbalimbali walioshiriki katika kufanikilisha tamasha kubwa la kwanza la kimataifa la kuifadhi Quan tukufu lilofanyika katika uwanja wa Benjamini mkapa jiji Dar es salaam.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vyeti hivyo iliyofanyika makao makuu ya bakwata jijini dar es salaam, alisema kwa kipekee anamshukuru Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Samia Suluhu Hassan kwa ushirikiano aliowata ngau awali pamoja na kuridhia ombi la kuwa mgeni rasmi siku ya mashindano.

Alisema mheshimiwa rais pamoja majukumu mazito ya kitaifa lakini akusita kuweza kutoa mchango wake kubwa ambao ulipelekea kufanikisha tamasha hilo kubwa la kwanza sambamba na kukubali ombi la kuwa mgeni rasmi.

“Kipekee ntoe shukrani kwa mheshimiwa rais Dokta Samia Suluhu Hassan kwa mchango mkubwa aliotupatia kuandaa tukio hili muhimu ikiwa ni pamoja na kukubali ombi la kuwa mgeni siku ya mashindano makubwa ya kwanza ya kimataifa ya kuhifadhi Quan pamoja na majulumu mengi ya kitaifa aliyonayo” Alisema Mufti Dkt. Abubakar.

Katika hatua nyingine mufti pia ameyashukuru mashirika pamoja na taasisi mbalimbali ambazo zilishiriki kwa namna moja au nyingine katika kuhakikisha kuwa mashindano hayo ya kwanza ya kuhifadhi Quan yanafanikiwa.

Amezitaja taasisi hizo ambazo zilikuwa sambamba na kutoa mchango kubwa katika kuhakikisha kuwa mashindano hayo yanafanikiwa kuwa ni Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Dar es slaam, wakuu wa wilaya zote za mkoa wa dar es salaam, viongozi wa dini ya kiislam kutoka ngazi mbalimbali wakiongozwa sheikh wa mkoa wa dar es salam walid alhad.

Amezitaja taasisi nyingine kuwa ni Taasisi za kidini, mshrikika na makampuni binafsi, mabalozi wanaowasilisha nchi zao nchini pamoja na vyombo vya habari.

 

No comments