Lulu Ateuliwa Kuwa Balozi Tamasha La Kimataifa La Sinema Zetu.
Balozi wa sinema zetu, Elizabeth Michael akizungumza katika mkutano na
waandishi wa habari (hawapo pichani), kushoto ni mwenyekiti wa tamasha hilo Profesa Martin Mhando, festival director Jacob joseph
Msimamizi wa Chaneli hiyo ambaye pia ni Mratibu wa tamasha hilo Zamaradi Nzowa akifafanua jambo katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.
Dar
es salaam:
KITUO cha Runinga cha Azam kupitia Chaneli 103 kimemteua Msanii wa
maigizo nchini, Elizabeth Michael 'Lulu' kuwa Balozi wa Maonyesho ya Tamasha la
Kimataifa la Sinema Zetu linalotarajiwa kuanza mwezi Januari hadi Aprili
Mosi mwakani.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Msimamizi wa chaneli
hiyo ambaye pia ni Mratibu wa tamasha hilo Zamaradi Nzowa wakati akiwafafanulia
wanahabari kuhusu mcahakato mzima wa kupata filamu zitakazoshindanishwa.
Amesema wamemteua muigizaji huyo kuwa balozi wa tamasha hilo
kutokana na kuianza sanaa hiyo siku nyingi tangu akiwa mtoto mdogo huku
akibainisha lengo lake ni kutoa wigo mpana kwa wasanii wa maigizo kujitangaza
kimataifa.
" Lulu ameteuliwa kuwa balozi kwa sababu ni msanii aliyeanza
maigizo siku nyingi tunaamini atalitangaza tamasha tunaamini kupitia yeye watu
wengi wataangalia tamasha litakalokuwa na manufaa kwa wasanii wetu,"
amesema Zamaradi.
Akizungumza mara baada ya kutangazwa kuwa balozi wa tamasha hilo Msanii Elizabeth Michael (Lulu) alisema katika tamasha hilo kutakuwa na vipengele mbalimbali
vikiwemo vya Filamu bora itakayozawadiwa Sh milioni 1.5, Filamu fupi Sh milioni
1.5, Muigiaji bora wa fialmu ndefu Sh milioni tano, filamu fupi Sh milioni 1.5,
Muigizaji bora wa Makala Sh milioni tano, muigizaji wa bora wa kiume na wa kike
wa filamu ndefu watazawadiwa Sh milioni tano kila mmoja.
Lulu aliongeza kuwa pia Mchekeshaji bora atakeyapata sh
milioni 2, Mwandishi bora wa filamu nddefu Sh milioni mbili na wa fupi sh
milioni moja, Wahariri wa filamu ndefu Sh milioni mbili, Muingizaji mziki wa
filamu ndefu sh milioni mbili wa fupi sh milioni moja.
Amezitaja zawadi nyiningine ni kwa mpiga picha bora wa
filamu ndefu sh milioni mbili huku wa fupi atapata sh milioni moja, makala
inayozungumza utaifa sh milioni moja pamoja na watazamaji kupata fursa ya
kuchagua filamu bora itakayopata sh milioni moja.
No comments