Breaking News

Dc Mjema Aingilia Kati Ugomvi wa FFU na Wananchi wa Ukonga Dar

Mkuu wa wilaya ya Ilala ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama Mhe. Sophia Mjema akiongea na wananchi wa eneo la Ukonga Mazizini mapema leo Jijini Dar es salaam.

Wakazi wa eneo la ukonga mazizini walilojitokeza kumpokea mkuu wa wilaya ya ilala ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama Mhe. Sophia Mjema kufatia kupigwa na kuporwa mali zao na watu wanaosadikiwa kuwa ni askari wa FFU.

Wakazi wa Ukonga Mazizini wakishangilia baada ya Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema, kuwataka wale wote walijeruhiwa kuandika majina yao hili taratibu za kuwapatia matibabu zianze mara moja sambamba na kuhaidi kuwa wahusika wa tukio hilo wote watachukuliwa hatua za kisheria.

Dar es Salaam:
MKUU wa Wilaya ya Ilala, ambaye ni mwenyekiti ya kamati ya ulinzi na usalama Mhe.Sophia Mjema amewapiga marufuku askari wa kikosi cha FFU na kusema hataki kuwaona wakisumbua wananchi katika eneo la Ukonga Dar es Salaam na kutaka waliohusika wachukuliwe hatua kwa kitendo walichofanya kuwapiga wananchi.

Akizungumza na wananchi alipowatembelea mapema leo na kujionea hali halisi wananchi wamelalamika kufanyiwa fujo na kupigwa na askari hao kwa siku mbili kutokana na askari mmoja kuuwawa na watu wasiojulikana.

Alisema askari hao walipaswa kufanya uchunguzi kujua ni watu gani walihusika kufanya mauaji ya askari huyo na si kwenda kufanya fujo na kuwapiga wananchi pasipokuwa na sababu

"Kama kuna askari alipatikana ameshafariki utaratibu ulikuwa uchunguzi ufanyike ili waweze kujiridhisha baada ya hapo wale ambao wangetambulika ndiyo wangechukuliwa hatua lakini kwa hili halikubaliki, kwa hiyo nasema hivi askari wote waliohusika kufanya fujo na vurugu wachukuliwe hatua za kinidhamu na huku barabarani sitaki kuona FFU yoyote anasumbua wananchi" alisema Mhe Mjema.

Aidha Mhe. Mjema ametaka wananchi ambao wameumizwa na askari hao kwa vipigo kwa siku mbili mfululizo waweze kujiorodhesha kwa majina ili wapatiwe matibabu na kusema wale ambao wamepoteza mali zao utaratibu utafanyika kuona nini kifanyike

No comments