Watetezi haki za binadamu waitaka serikali kuzingatia misingi ya demokrasia, utawala wa sheria kutekeleza majukumu yake.
Mtandao wa mashirika
ya Watetezi wa haki za binadamu nchini umeitaka serikali ya Jamhuri ya muungano
wa Tanzania kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia misingi ya demokrasia na
utawala wa sheria ikiwemo uhuru wa vyama vya siasa.
Akisoma tamko la
wadau hao katika kilele cha Maadhimisho ya siku ya Amani duniani ambayo
udhimisha kila mwaka tarehe 21 septemba, Mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki
za binadamu Dkt. Helen Kijo bisimba alisema amani ujengwa kwa kwa kufuata
misingi ya tawala bora pamoja na kuzingatia misingi ya demokrasia.
Alisema misingi amani
iliyopo nchini imechangia ustawa wa taifa kijamii, kisiasa na kiuchumi pamoja na
kuwajengea watanzania utashi wa utu, mshikamano na uzalendo pamoja na kuwepo
changamoto ambazo tunaendelea kuzikabili.
“Tunawapongeza
watanzania kwa kuweza kudumisha amani yetu kwa miaka zaidi ya 50 tangu
tulipopata uhuru 1961 na hata tulipongana na Zanzibar 1964 na hata mara baada
ya kurejesha mfumo wa vyama vingi nchini” Alisema Dkt Bisimba.
Alisema pamoja na jitihada
zote zinazochukuliwa za kuendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano uliopo
nchini mashirika ya utetezi wa haki za binadamu wamebaini kuwepo na viashiria vinavyoweza
kupelekea kutoweka kwa amani iliyopo nchini.
Amevitaja viashiria
hivyo kuwa ni matumizi mabaya ya madaraka na ukiukwaji wa utawala wa kisheria,
kuongezeka kwa vitendo vinavyotia hofu kuhusu amani na ulinzi wa haki za
binadamu, matukio ya ukamatwaji kihilela kwa wanasiasa na wafuasi hasa wa vyama
vya upinzani pamoja na kuminya uhuru wa habari na uhuru wa maoni.
Alisema kufatia
kubaini viashria hivyo mtandao wa mashirika ya watetezi wa haki za binadamu
umeshauri vyombo vya usimamizi wa sheria kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi,
wakati na weledi ili kuepusha malalamiko kutoka kwa wananchi.
Aidha Dkt. BIsimba
aliongeza kuwa serikali ichukue hatua za makusudi za kuhakikisha ustawi wa umoja
wa kitaifa kwa kuyaunganisha makundi yote yanayosigana kisiasa, kijamii na
kiuchumi.
Maadhimisho ya siku
ya Amani duniani ambayo uadhimishwa kila mwaka tarehe 21 septemba, mwaka huu
2017 yamebeba kauli mbiu ya “Pamoja Kwa Ajili Ya Amani: Nizamu, Usalama
Na Heshima Kwa Wote”.
No comments