TANZIA: MKE WA MZEE YUSUF 'BI CHIKU' AMEFARIKI DUNIA
Habari zilizonifikia muda huu kutoka Dar
es salaam ni kuhusu kifo cha mke mdogo wa Mwimbaji wa zamani wa Jahazi Modern
Taarabu Alhaj Mzee Yusuph Chiku amefariki usiku huu wakati anajifungua na mtoto
naye amefariki.
Kupitia matandao wa Instagram Mtangazaji wa Clouds
FM Geah Habib ameandika:
>>>”Innalillah wainaillah rajuun
mke mdogo wa Mzee Yusufu #Chiku amefariki dunia
usiku huu alipokuwa akijifungua na mtoto amefariki taarifa zaidi tutaendelea
kupeana!!” – Geah Habib.
Chiku amekutwa na mauti leo Jumamosi June
17,2017 jioni katika hospitali ya Amana, Ilala ya jijini Dar es Salaam
alipopelekwa kujifungua.
Mzee Yussuf amesema alimpeleka mkewe
Hospitalini hapo June 17, 2017 saa 10 alasiri kwa ajili ya kujifungua na kwa
bahati mbaya alikutwa na mauti hayo baada ya upasuaji uliofanywa kutokwenda
salama hivyo
kusababisha kumpoteza mkewe na mtoto
aliyezaliwa.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA
PEPONI..AMINA.
No comments