Breaking News

DC HAPI AFUNGUA MKUTANO WA KWANZA WA BARAZA LA BIASHARA WA WILAYA YA KINONDONI ASISTIZA UMAKINI KATIKA KUKUSANYAJI WA MAPATO

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akifungua mkutano wa kwanza wa wa baraza la biashara wa wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam.



Washiriki wa mkutano huo wa baraza la biashara wilaya ya kinondoni kutoka taasisi mbalimbali jijini Dar es saalm.

 Washiriki wa mkutano huo wa baraza la biashara wilaya ya kinondoni kutoka taasisi mbalimbali jijini Dar es saalm.

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Hapi ameitisha mkutano wa kwanza wa baraza la biashara wa wilaya ya Kinondoni ili kujadiliana na wafanya biashara  kuhusu masuala ya biashara.
Akizungumza jijini Dar es salaam Mhe Hapi ambaye ni mwenyekiti wa baraza la biashara alisema lengo la kukutana  na wadau hao ni kutoa fursa kwa wafanyabiashara na mamlaka husika kujadili changamoto zinazowakabili na kutathmini mwenendo mzima wa biashara.
Alisema kumekuwepo na changamoto kubwa katika ukasanyaji wa mapato hasa kwa wadaiwa sugu kutotaka kulipa kodi hivyo kuziagiza mamlaka husika kuimarisha mfumo  mzima wa ukusanyaji kodi.
“ili nchi ikue kiuchumi amewaagiza maofisa biashara kutekeleza agizo lililotolewa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuhusu wamachinga wote kutambuliwa kwa kupewa vitambulisho na kulipia kisheria hivyo ni vema kuwekewa utaratibu huo badala ya kujikuta wakitapeliwa hovyo na matapeli” alisema Mhe Hapi
Aidha amewaomba wananchi kuwafichua watendaji wa serikali ambao wana tabia za kutoa kauli za vitisho au kukatisha tamaa kwa wafanyabishara wakati wa kukusanya malipo ya kodi.
Pia mhe Hapi  amewaonya wale wote wanaoghushi leseni za biashara au nyaraka za serikali kuacha mara moja kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria na kuwa hatua kali zitachukuliwa wakibainika.




No comments