Breaking News

WATUMIAJI WA HUDUMA ZA TRENI ZA ABIRIAWATAKIWA KUZINGATIA SHERIA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 
Watumiaji wa huduma za usafiri wa treni za abiria za Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) wametakiwa kuzingatia sheria za matumizi ya usafiri huo ili kuepuka adhabu ya kufungwa jela miezi sita.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka uongozi wa TRL umeainisha kuwa matumizi ya usafri wa abiria unasimamiwa na sheria,kanuni ,taratibu na masharti maalum. Mojawapo limetajwa ni kutodandia mabehewa baada ya milango kufungwa.

Uongozi katika taarifa hiyo umesisitiza kuwa endapo mtu atafanya kosa hilo atafikishwa mahakamani na kuhukumiwa kifungo kisiochopungua miezi sita.

Taarifa hii imetolewa baada ya kuonekana kushamiri vitendo vya kuvunja taratibu za usalama za usafiri wa treni.

Aina hii ya uvunjaji huo wa matumizi yasiyo salama mwaka jana Agosti 03, 2016 yalisababisha , mtu mmoja kupoteza maisha baada ya kugongwa na geti la lango la kuingilia treni Stesheni.

Marehemu alikuwa akinining’inia nje ya behewa wakati wa treni ya Pugu majira ya jioni ikiingia ndani ya eneo la kituo kikuu cha Dar es Salaam.

Uongozi wa TRL umefafanua kuwa tofauti ya usafiri wa basi ni kwa vile kondakta anaweza kusimamisha basi ili kumshusha mtu anayening’inia nje lakini kwa treni jinsi ilivyo ndefu hilo haliwezekani kufanyika kirahisi.
.
Aidha katika taarifa hiyo Uongozi uimetoa wito kwa wasafiri na wananchi kwa jumla kufuata masharti ya usafiri wa treni za jiji hasa wale wanao tumia treni ya iendayo Pugu. 

Ili kuepuka maafa na pia kuchukuliwa hatua za kisheria ambazo zitasababisha mkosaji kufungwa jela..

Wakati huo huo Kikosi cha Polisi Reli kimeanza operesheni ya kuwadhibiti abiria ambao hawataki kufuata sheria, kanuni na taratibu za matumizi ya usafiri salama wa treni na hasa kwa kuning’inia nje ya mabehewa wakati treni ikitembea. 

Aidha operesheni hiyo itahusisha kuwafikisha mbele ya sheria wasafri wote watakaokamatwa wakienda kinyume na masharti ya usalama wa usafiri wa reli.

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano:
Kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL
Ndugu Shaban Jumbe Kiko,
Mei 17, 2017
DAR ES SALAAM

No comments