Breaking News

WAZIRI UMMY: TUWAJALI NA KUWASAIDIA BADALA YA KUWATENGA NA KUWAKEJELI WANAWAKE WENYE FISTULA

Jamii imetakiwa kuwajali na kuwasaidia badala ya kuwatenga na kuwakejeli wanawake wenye fistula kwani kwa kufanya hivyo kuwatawasaidia kujiona kuwa moja sehemu ya jamii.

Akizungumza mapema leo jijini dar es salaam Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema hipo haja kwa jamii kutambua umuhimu wa kuwajali, kuwatunza na kuwaonyesha upendo wanawake wenye ugonjwa huo.

Alisema Tanzania ni moja ya nchi iliyo na wanawake wengi wenye fistula na jamii imekuwa ikiwatenga jambo ambalo limechangia wengi wao kukosa matibabu na hivyo kuishi na ugonjwa huo kwa muda mrefu.

Waziri ummy alisongeza kuwa hili kutokomeza ugonjwa huo inaitajika nguvu za pamoja hususani kwa jamii kuwasaidia serikali kuhakikisha wagonjwa wa fistula wanafika katika vito vya afya hili kupatiwa huduma kwa haraka zaidi tofauti na ilivyo sasa.

“Wanawake wawe wanajitahidi kufika katika vituo vya afya kwa haraka lakini pia jamii iwasaidie wapate huduma ili wapone, tofauti na ilivyo sasa kutokana na sehemu kubwa ya jamii bado wanawatenga” alisema waziri Ummy.

Aidha waziri ummy aliongeza kuwa serikali katika kuhakikisha inatokomeza ugonjwa wa fistula nchini katika bajeti bajeti ya fedha ya mwaka huu imepanga kuongeza vituo vya afya 100.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA), Dk. Hashina Begum alisema lengo la UNFPA kwa kushirikiana na serikali pamoja na wadau wengine wa afya uhakikisha wanatokomeza ugonjwa wa fistula nchini.


Alisema UNFPA ikichukua hatua za makusudi katika kuhakikisha wanatokomeza ugonjwa wa fistula nchini na kutolea mfano mwaka uliopita pekee zaidi ya wanawake 1,356 wenye ugonjwa huo walisaidiwa kufanyiwa  upasuaji.