Breaking News

ITEL MOBILE TANZANIA YAMTANGAZA MSANII IRENE UWOYA KUWA BALOZI WAKE NCHINI.

 Mwakilishi kutoka Itel Mobile Tanzania Bw Cooper Chen Ikizungumza katika mkutanoa wa kumtambilisha balozi wa ITEL Mobile Tanzania pamoja na kutambulisha simu ya ITEL S31.
Bolozi wa ITEL Mobile Tanzania Irene Uwoya Akizungumza mara baada ya kutangazwa kuwa balozi wa kampuni hiyo.
Wa kwanza kuanzia kushoto Bw Aloyce Michael akishaudia uwekaji wa saini makubaliano, wa pili kutoka kushoto Balozi wa ITEL Mobile Irene Uwoya, Mwakilishi wa ITEL Mobile bw Cooper Chen na wa kwanza kilia Bi Asha Mzimbili.

 Balozi wa ITEL Mobile Irene Uwoya na Mwakilishi wa ITEL Mobile bw Cooper Chen wakikabidhiana makubaliano mara baada ya kutiliana saini.
Meneja masoko Wa ITEL Mobile Tanzania Bw Wolle Fernando akifafanua jambo katika halfa hiyo.


Washiriki na wadau kutoka sehemu mbalimbali waliohudhulia halfa hiyo wakipiga piga na balozi wa ITEL Mobile Tanzania Irene uwoya.

Dar es salaam.
Kampuni ya ITEL Mobile Tanzania leo imezindua simu mpya aina ya ITEL S31 (Selfie In Low Light) sambamba na mtambulisha balozi wa bidha zake hapa nchini muigizani Irene Uwoya.

Akizungumza mapema leo jijini dar es salaam katika hafla ya uzinduzi huo pamoja na kumbabulisha balozi wa bidhaa zake nchini Meneja Masoko wa ITEL Mobile Tanzania Bw Wolle Fernando Alisema wamekuwa mstali wa mbele katika kuzalisha vifaa bora ambavyo vitawapatia wateja wao mawasiliano ya kiwango cha juu cha ubora.

Alisema kampuni kwa kutambua hilo ITEL Mobile Tanzania imeamua kuingia makubaliano na msanii maarufu wa filamu nchini Irene Uwoya kuwa Balozi kwa kipindi cha mwaka mmoja ili kupitia yeye ataweza kuunganisha Itel Mobile na watanzania.

Bw Fernando aliongeza kuwa katika kipindi hicho cha mwaka mmoja jamii itafaidika na kupata elimu juu ya bidhaa zao hususani kupitia Program wanazozifanya za kusaidia makundi mbali mbali ya kijamii za Charity Event Programs.

Akizungumzia simu ya ITEL S31 Bw Fernando alisema kampuni ITEL Mobile mara zote imekuwa mstali wa mbele katika kutengeneza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu ambazo zinakidhi mahitaji ya wateja wao.

Alisema simu ya ITEL S31 imetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu ikiwa na uwezo wa kutunza na kukaa na chaji kwa kipindi kirefu, kioo chenye ukubwa wa 5.5 Hd, kamera yenye ubora wa kupiga picha katika mwanga hafifu (Selfie yenye Flash) pamoja na Memory ya ndani ya simu yenye ukubwa wa 16GB.

Kwa upande wake balozi wa ITEL Mobile Tanzania Irene Uwoya alisema ni faraja kwake kutokana na kampuni hiyo kutambua mchango wake kwa jamii hivyo anaona fahari kufanya kazi na kampuni hiyo ukizingaitia ubora wa bidhaa zake inazozizalisha.

“Najisikia faraja sana kuteuliwa kuwa balozi wa ITEL Mobile Tanzania kutokana na ubora wa bidhaa zao wanazozalisha kwa kipindi cha miaka 10 tangu kuanza kutoa huduma zao nchini hivyo natoa wito kwa watanzaania kutumia simu za ITEL Mobile hususani ITEL S31 Hili weweze kufurahia ubora wake” Alisema Uwoya