Breaking News

UKARABATI WA RELI KUPUNGUZA SAFARI ZA TRENI YA JIJI KUTOKA DAR KWENDA PUGU KUANZIA 2 JANUARI 2017

Kampuni ya reli nchini (TRL) imetangaza kuanza kufanya  maboresho ya reli yake kwa kiwango cha ratili 80 kutoka kituo kikuu cha Dar es salaam mpaka Pugu kuanzia jumatatu ya januari 2 mwaka 2017.


Akizungumza mapema leo jijini dar es salaam, Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uendeshaji wa kampuni ya Reli nchini (TRL) Ndugu Focus Sahani alisema kuanza kwa mradi huo wa kutandika reli za uzito wa ratili 80 na kuondoa zile nyepesi za ratili 60 kuanzia Kituo kikuu cha Dar es Salaam mpaka Pugu umbali wa kilomita 20.4 umelenga kuboresha utoaji wa huduma za usafiri huo kwa ufanisi zaidi. 
Amesema kuanza kwa ukarabati wa njia hiyo ambao utachukua takribani wiki 10 mpaka kukamilika kwake utapelekea kupunguzwa safari 2 za treni ya Jiji kwenda Pugu  ambazo ni Safari ya mwisho asubuhi ya 3:15 na ile ya mwisho usiku saa 2:45,

Aidha amezitaja  Faida itakayopatikana baada ya kazi hiyo ni reli kuimarika ni kupunguza kutimka vumbi kama ilivyo sasa wakati treni ikiwa inatembea  na kuongeza kuwa  Kokoto zitakazotumika katika ujenzi huo ni maalum hazitoi vumbi wakati treni ikipita.

No comments