SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR YAWEKA KIPAUMBELE SEKTA YA UTALII.
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
imeamua kuweka kupaumbele mbele sekta ya utalii kwa kuwashirikisha
wananchi katika mpango wa kutekeleza sera ya utalii kwa wote.
Hayo ameyasema Mwenyekiti wa
Kamisheni ya Utalii Dr. Ahmada Hamadi Khatib leo huko katika ukumbi wa
sanaa wa Studio ya Sanaa Rahaleo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya
watembezaji Utalii nchini.
Amesema Utalii unahitaji
kushirikiana sekta ya Habari , Utamaduni na Michezo ili kuweza kupata
mashirikiano katika taasisi zote katika kukuza utalii nchini na kuleta
maendeleo kwa Taifa.
Aidha amewataka watembezaji
watalii hao kuzingatia maelekezo wanayofundishwa katika kutekeleza
majukumu yao kwa lengo la kuimarisha na kudumisha amani na usalama
wakati wanapokuwa katika kazi yao ya kutembeza watalii.
Pia amesema ili uwe muongozajii
bora ni lazima ujue unachokiongoza , kwani watalii wanatarajia kuongozwa
na kufahamishwa sehemu mbali mbali za kihistoria na kutegemea kupata
maelekezo kwa ufasaha zaidi.
“Watalii wanapokuja Zanzibar
kutoka sehemu mbalimbali wanajua wanakuja hapa kwanza watu wake wakarimu
,tabia zetu nzuri na pia hulka zetu nzuri hivyo wajitahidi wawe
watembezaji wazuri waepuke kuwafanyia udanganyifu ambao utawasababishia
kuondosha uaminifu na kuondosha sifa ya Zanzibar”, amesema mwenyekiti
huyo.
Sambamba na hayo amesema
muongozaji mtalii anatakiwa kuwa na taaluma nzuri ambayo ataweza
kufanya wajibu wake na kufuatilia sehemu muhimu ambazo wanazopenda
kutembelea watalii.
Amewasisitizawatembezaji hao
kufuata matakwa watalii wanapohitaji kupelekwa sehemu na sio kufanya
wanavyotaka wao kwani kuwafanyia hivyo sio ustarabu na kwenda kinyume na
maadili ya kazi zao.