Breaking News

Jukata Yalaani Vikali Kupigwa Risasi Mhe Tundu Lissu… Watoa Neno Juu Ya Kwamo Wa Katiba Mpya.

Image result for PICHA YA Mkurugenzi mtendaji wa Jukwaa la katiba Tanzania Bw Hebron Mwakagenda
Jukwaa la katiba tanzania (JUKATA) limelaani na kusikitishwa na tukio la kupigwa na Risasi kwa mbunge wa singida mashariki na mwenyekiti wa chama cha wanasheria nchini (TLS) Mhe Tundu Lissu lililotokea mjini Dodoma mapema tarehe 7 mwezi huu.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi mtendaji wa Jukwaa la katiba Tanzania (JUKATA), Bw Hebron Mwakagenda alisema kwa mujibu wa taarifa mbalimbali zilizoripotiwa juu ya kushambuliwa kwa Mhe Lissu tumesikitishwa na kushangazwa na uonevu aliofanyiwa mbunge huyo.

“Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali ambazo zimekuwa zikiripotiwa na vyombo vya habari juu ya tukio hilo ni fedheha kwa taifa ambalo linajulikana duniani kote kama kisiwa cha amani tukio la kumshambulia mtu asiye na hatia kwa risasi zaidi ya 30 sio utamaduni wetu kama taifa” Alisema Bw Mwakagenda.

Alisema kufatia tukio hilo na mengine mengi ambayo yamekuwa yakiripotiwa nchini kama kuteka, kuwatesa na kushambuliwa kwa risasi yanayofanywa na watu wasiojulikana kuendelea kushamili wanatoa wito kwa vyombo vya dola kufanya kazi yake na wahusika wafikishwe mbele ya sheria.

Pia JUKATA limeitaka serikali kuchukua hatua za makusudi kukomesha matukio hayo ambayo yameanza kuota mizizi nchini hivyo kutia doa taifa kutokana miaka mingi kujulikana kama kisiwa cha amani.

Akizungumzuia kwamo wa mchakato wa katiba mpya Bw. Mwakagenda alisema JUKATA wamekuwa wakifatilia na kuzichambua Bajeti ya wizara ya katiba na sheria kwa mwaka fedha (2016/17 na 2017/18) wamebaini serikali aijatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha mchakato huo na wala hakuna maelezo ya kina juu ya hatma ya mchakato huo.

Alisema pamoja na watumaini ya watanzania walio wengi kuwa mchakato wa katiba mpya ungeweza kukamilishwa katika kipindi cha kwanza cha utawala wa serikali ya awamu ya tano chini ya Mhe Dkt. John Pombe magufuli kwasasa yameanza kufifia kutokana kutotengewa fedha yoyote katika bajeti ya serikali.

Alisema ikitokea hakuna uwezekano wa kukamilisha mchakatio wa katiba mpya kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 kama dalili zinavyo onyesha yafanyike marekebisho ya msingi ( Minimum Reforms) katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Alisema vifungu vya sheria zote zihusuzo uchaguzi vifanyiwe marekebisho hili kuondoa kasoro ambazo zimekuwa zikilalamikiwa karibu kila uchaguzi ambavyo ni uhuru kamili wa tume ya taifa ya uchaguzi Tanzania bara na Zanzibar na Uwezekano wa kuhoji matokeo ya uchaguzi mahakamani.

Amevitaja vifungu vingine kuwa ni kuwepo na fursa ya mgombea huru, vyama vya siasa kuungana, kurejesha mfumo wa ushindi katika uchaguzi wa rais kupatikana kwa kigezo cha kura zisizopungua asilimia 50.

Pamoja na kuingizwa katika katiba sheria ya usawa wa kijinsia katika uchaguzi na katika vyombo mbalimbali vya maamuzi kama mabaraza ya madiwani, bunge na baraza la wawakilishi.

No comments