RITA KUZIFUTA BODI ZA UDHAMINI ZENYE MAKOSA
Waziri
wa Katiba na sheria Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Mara
baada ya kupokea ripoti ya ukaguzi
kutoka Taasisi zote zinazofanya usajili wa Asasi za kiraia mapema leo jijini
Dar es Salaam. Kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Katiba na Sheria Amon Mpanju.
Katiba na Sheria Amon Mpanju.
Waandishi
wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa katika mkutano huo mapema hii leo jijini
Dar es Salaam.
Na
Frank Wandiba
Serikali
imesema itaendelea kuzikagua na kuzifanyia uhakiki bodi zote zilizo chini ya
Wakala wa Ufilisi na udhamini (RITA).
Waziri
wa sheria na katiba mhe Harrison Mwakyembe alisema hayo jijini dar es salaam
mara baada ya kukabidhiwa Ripoti ya ukaguzi wa taasisi wenye lengo la
kuzitambua taasisi zote zilizosajiliwa na kutambuliwa na RITA.
Alisema
ripoti hiyo licha ya kuziorodhesha taasisi
ambazo zinatambulika kisheria na kukidhi vigezo, pia ripoti hiyo itazionyesha
tasisi ambazo hazikidhi vigezo vya kisheria hivyo kufutwa na kubaki na taasisi zilizosajiliwa
na kutambulika kisheria.
Mapema
akielezea ripoti hiyo kaimu msajili wa vyama vya kiraia Bi, Marlin Komba
alisema taarifa ya bodi ya wadhamini inaonyesha kuwa wadhamini 1944 kati ya
5262 ziliwasilishwa kwa barua pepe (email), huku zingine zikiwasilishwa ofisi.
Alisema
kati ya majalada 5262 yaliyowasilishwa majalada 4287 yalichambuliwa na kuwekwa
katika kanzi data na kubainika kuwa bodi za wadhamini 500 zilikuwa mfu.
Katika
tangazo lililotolewa mei 17 mwaka huu kwenye gazeti la serikali la Daily News
pamoja na gazeti la Mwananchi kwa muda wa siku 30, kati ya taasisi 200 ni
tasisi 20 tu ndio azikuweza kutekeleza agizo hilo huku taasisi 180 zilibainika
kuwa zinatekeleza wajibu.
Aidha
ameongeza kuwa taasisi hiyo ina mpango wa kuzifuta taasisi 320 zoezi
litakalofanyika mapema mwezi Agost mwaka huu.
|
No comments